Wito huo ulitolewa na Ndugu Hamad Kibwana, ambaye alimwakilisha Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wilayani humo, katika kikao kazi kilichofanyika kwenye ukumbi wa Sky Way. Alisisitiza kuwa jukumu la kuzuia rushwa ni letu sote, na njia mojawapo ni kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa miradi hii ili kuhakikisha thamani halisi ya fedha za umma inapatikana.
Kikao hicho muhimu kiliongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mheshimiwa Denis Masanja, na kiliwaleta pamoja watumishi katika ngazi za utawala wa wilaya. Madhumuni yake yalikuwa kuwajengea uelewa watendaji hawa kuhusu majukumu yao katika kusimamia maendeleo na kupambana na vitendo vya rushwa vinavyoweza kujitokeza kwenye miradi. Hii inajumuisha kuhakikisha taratibu zote za manunuzi na utekelezaji zinafuatwa bila upendeleo.
Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mheshimiwa Denis Masanja, amekabidhi hati za kimila 472 kwa wananchi wa Kijiji cha Ngapa. Mpango huu una lengo la kuleta utulivu na maendeleo kwa jamii. Utekelezaji wake unalenga kuondoa migogoro ya ardhi na kuimarisha usalama wa umiliki wa ardhi miongoni mwa wananchi, ambao mara nyingi wamekuwa wakikumbana na changamoto mbalimbali.
Akitoa taarifa kwa Mkuu wa Wilaya, ndg Stephen Mpondo Afisa Mahusiano Jamii kutoka Hifadhi ya Taifa Nyerere (W),alizungumza kwamba, Jumla ya hati 2,783 zimetayarishwa kwa ajili ya vijiji nane vilivyopo katika Wilaya ya Tunduru vyenye mipango ya matumizi ya ardhi, kupitia mradi wa ERB unaosimamiwa na Hifadhi ya Taifa ya Nyerere. Kati ya hati hizo, Kijiji cha Ngapa pekee kimepokea hati 472. Vijiji vingine vilivyofaidika ni Muhuwesi (hati 291), Mnazi Mmoja (hati 355), Liwangula (hati 312), Chawisi (hati 225), Jaribuni (hati 314), Matemanga (hati 156), na Ligunga (hati 658). Mpango huu unaonesha dhamira ya serikali ya kuboresha maisha ya wananchi wake kupitia urasimishaji wa umiliki wa ardhi.
Mikopo hiyo ya shilingi milioni 574,257,500 imelenga makundi yenye mahitaji maalum ya kiuchumi. Kwa ujumla, vikundi 50 vya wajasiriamali wadogo vimenufaika na fedha hizi. Vikundi hivyo vimegawanyika katika makundi makuu matatu: vikundi 24 vya wanawake, vikundi 21 vya vijana, na vikundi 5 vya watu wenye ulemavu. Jumla ya wanufaika ni 227
Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.