• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WAMAMA MASHUHUDA watoa siri ya afya bora ya watoto kupitia maziwa ya mama pekee Tunduru.

Imewekwa : August 1st, 2025

Mama Nasra Juma,Bi Zawadi na Bi Namsifu ni miongoni mwa wanawake wajasiri walioshiriki katika hafla ya uzinduzi wa Wiki ya Unyonyeshaji Tunduru, ambapo walisimama kama mashuhuda na kuwahimiza kina mama wenzao. Kwa kujiamini na furaha, walieleza jinsi walivyonyonyesha watoto wao maziwa ya mama pekee kwa miezi sita ya mwanzo bila kuwapatia maji wala chakula kingine.

Mama Nasra Juma, mkazi wa Tunduru, ni mmoja wa akina mama waliosimama na kutoa ushuhuda wa jinsi alivyonyonyesha watoto wake wawili maziwa ya mama pekee kwa miezi sita ya mwanzo. Kwa tabasamu na uso wenye nuru, Mama Nasra Juma alisimulia safari yake: "Nilifuata ushauri wa wataalam wa afya na nikajizuia kabisa kumpa mtoto wangu maji, chai, au uji katika miezi sita ya kwanza. Watu walinishangaa, wengine walisema nitamtesa mtoto wangu, lakini nilisimama imara. Matokeo yake, mtoto wangu alikua na afya njema, hakuugua mara kwa mara, na ana akili timamu. Ninafurahi kuona ni mzima kabisa."

Ushuhuda huu uliungwa mkono na mama mwingine, Bi. Zawadi, ambaye alisisitiza umuhimu wa akina mama kuamini maziwa yao wenyewe. "Ninaona fahari sana ninapowaangalia watoto wangu wawili wakubwa ambao wote niliwanyonyesha kwa miezi sita ya kwanza bila kuwapa kingine. Hii inawezekana kabisa. Nawaomba wamama wenzangu msidanganyike na maneno ya mtaani. Kuwanyonyesha watoto wenu maziwa ya mama pekee kwa miezi sita ya kwanza si kuwatesa, bali ni kuwajengea afya imara kwa maisha yao yote,"

Akithibitisha kuwezekana kwa suala hili, Afisa Biashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, Bi. Namsifu alikazia msimamo wa serikali katika kuwezesha unyonyeshaji. Alifafanua kuwa licha ya shughuli nyingi za kiofisi, serikali imeweka sheria na miongozo inayomruhusu mama kupewa muda wa kutosha wa likizo ya uzazi na pia kupata muda wa kutosha kazini ili aweze kunyonyesha mtoto wake kwa miezi sita ya kwanza bila bughudha. Alisisitiza kuwa lengo ni kuhakikisha kila mtoto anapata haki yake ya kupata lishe bora kutoka kwa mama yake, na hivyo kujenga kizazi imara na chenye afya.

Ushuhuda huu ulitoa hamasa kubwa kwa kina mama wengine waliohudhuria hafla hiyo, kuwathibitishia kwamba unyonyeshaji wa maziwa ya mama pekee kwa miezi sita inawezekana na matokeo yake ni mazuri kwa afya ya watoto.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.