• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Historia

HISTORIA YA WILAYA YA TUNDURU 


Wilaya ya Tunduru ilianzishwa mwaka 1905 kipindi cha utawala wa ukoloni ambapo Serikali ya Ujerumani ilijenga boma katika eneo la Kadewele karibu na lilipo jengo la Mamlaka ya Mapato (TRA) kwa sasa.

Wilaya hii ni miongoni mwa wilaya sita (6) za Mkoa wa Ruvuma, ambapo kwa upande wa Kaskazini inapakana na Mkoa wa Lindi,Mkoa wa Mtwara kwa upande wa Mashariki, Namtumbo upande wa Magharibi na Nchi ya Msumbiji kwa upande wa Kusini.

Kwa mujibu wa matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi iliyofanyika Agosti, 2020 idadi ya wakazi ilikuwa 412,054 kati yao Wanaume ni 201,668 na Wanawake ni 210,386. Sehemu kubwa ya wakazi wa Tunduru ni Wayao ambao wamehamia toka Nchi jirani ya Msumbiji. Makabila yanayopatikana Wilayani Tunduru ni pamoja na Wamakua, Wangoni, Wanindi, Wandendeule, Wamatengo na Wasukuma.

Wilaya ya Tunduru ina jumla ya Tarafa 7 na kata 39. Tarafa ni kama zifuatazo;-

  1. Namsakata
  2. Nampungu
  3. Nalasi
  4. Matemanga
  5. Nakapanya
  6. Lukumbule
  7. Mlingoti

Kuhamia kwa Wayao Tunduru.

Kati ya mwaka 1800 na 1900 Wayao wengi walihama Msumbiji kuelekea sehemu mbalimbali kama vile vile Malawi na Kusini ya Tanzania. Wakati wa Utawala wa Mwenye Mataka Nchini Msumbiji kulikua na vita vya mara kwa mara kati yake na Wareno. Ingawa mara nyingi alishinda, lakini baadaye alizidiwa nguvu na kulazimika kuvuka mto Ruvuma na kuhamia Boma la Tunduru mwaka 1912. Sultani Mataka alipokelewa na umati mkubwa wa ndugu zake waliotangulia, pia walikuwepo wazungu wawili wa Kijerumani ambao ni Mwana Kiliman-DC na Bwana Verde ambao waliondamana na Maakida kutoka mto Ruvuma mpaka kijiji cha Lipepo. Mwenye Mataka (Che Chisonga) alihamia na watu 10,000 na Mamwenye wasiopungua 32.

Kabla ya kuhamia rasmi Nchini Tanzania Sultani Mataka aliwatuma baadhi ya Mamwenye kuja kufanya upelelezi kuona kama maisha ya huku Tanzania yatawafaa. Baadhi yao ni pamoja na Mwenye Gwaya, Mwenye Kadewele, Mwenye Myao, Mwenye Mkwanda na Bibi Akundenda.

Mnamo mwaka 1889 – 1890 wajerumani walianza kujenga Boma karibu na mamlaka ya mapato (TRA) ilipo sasa. Makazi ya watu yakiwa sehemu za Mkwanda na kadewele.Wakati huo jina Likiwa Tunduru

Asili ya Jina Tunduru.

Mnamo mwaka 1860 Bibi Akwitundulu ambaye ni dada wa Akumachemba (Machemba) mmoja kati ya makamanda wa Sultani Mataka,alianzisha maskani yake sehemu iitwayo Malombe kusini Magharibi ya mji wa Tunduru umbali wa Km 5. Maskani yake yakastawi sana na kuwa kituo kikubwa cha biashara ya misafara kutoka Msumbiji hadi kilwa. Kwa kuwa Bibi Akwitundulu alikuwa hodari, mkarimu na mwenye upendo na mchangamfu kutokana na tabia hizo aliweza kuwatetea wasafiri wengi waliokuwa wanapita katika eneo lake walitokea jimbo la Nyasa Nchini Msumbiji au Pwani ya Kilwa kurejea Msumbiji.

 Sifa za Bibi Akwitundulu na kijiji chake zikaenea katika sehemu kubwa na hivyo watu wakaanza kuhamia na kufanya kijiji cha Malombe kuwa kituo kikubwa cha biashara ya misafara

Mnamo mwaka 1887 na 1888 Wajerumani walitembelea eneo la Malombe ,walipouliza ni watu gani wanaishia pale, wakaambiwa kuwa ni sehemu ya Bibi Akwitundulu, hivyo wao wakaita sehemu hiyo kuwa ni Tunduru kwa kushindwa kutamka Akwitundulu.

Bibi Akwitundulu alifariki dunia mwaka 1889 na kuzikwa hapo hapo kijijini pake karibu sana na kijiji cha Malombe

Boma la kwanza lilijengwa eneo la Mkwanda shughuli muhimu za biashara kama maduka makubwa yalijengwa, kwa sasa hivi eneo hilo hujulikana kama majengo ya zamani.

Utamaduni

kabila la wayao kama zilivyo jamii nyingi za mikoa ya kusini wakati wa mavuno wanakuwa na ngoma, na baada ya mavuno wengi wao huandaa sherehe za jadi maarufu kama Unyago. Ngoma hii huwa na lengo la kuwafundisha mabinti namna ya kukabiliana na changamoto za maisha hasa katika ndoa. kuna aina mbali mbali za ngoma kama Mabega, Mganda nk.

Hali ya hewa

Hali ya hewa ni ya joto la wastani wa nyuzijoto 25°c linalofaa kwa ustawishaji wa mazao mbalimbali. Wastani wa mvua ni milimita 960 kwa mwaka ambapo mvua hunyesha kuanzia mwishoni mwa mwezi Novemba hadi Aprili. Aina ya uoto ni Miombo. Hali ya udongo ni mchanga na mfinyanzi kwenye maeneo ya mabonde. Asilimia 30 ya vijiji ndani ya wilaya vina mito isiyokauka kwa mwaka mzima. Wilaya ya Tunduru ina mwinuko wa kati ya meta 200 na 500 kutoka usawa wa bahari na hali ya nchi ni ya tambarare na vilima upande wa Kusini Magharibi.

Shughuli za kiuchumi

Wilaya ya Tunduru ni wilaya ambayo shughuli kubwa za kiuchumi ni kilimo cha zao la biashara la korosho ambayo hulimwa karibu katika maeneo yote ya wilaya, pia watu wa Tunduru wanalima mazao mengine kama Mpunga, Mbaazi, Choroko, Kunde,Ufuta na Karanga.

Wilaya ya Tunduru ina vivutio mbalimbali vya utalii ambavyo ni Mbuga ya Wanyama Selous, mapori ya akiba ya Sasawala na Muhuwesi, masalia ya majengo ya wapigania Uhuru wa Msumbiji kupitia Chama cha Frelimo, makaburi ya viongozi wa kimila, Miti inayogeuka kuwa mawe, mapango ya ajabu na nyayo za wanyama katika mwamba vyote hivi ni sehemu ya utalii na vinapatikana katika wilaya ya Tunduru pekee.

shughuli nyingine za uchumi zinazofanywa na wananchi wa Wilaya ya Tunduru ni shughuli za biashara, ufugaji wa nyuki, kuku, Samaki, Mbuzi na Ngombe. Pia wanafanya biashara za aina mbalimbali katika mazingira yao.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.