• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

Imewekwa : May 7th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru leo imezindua rasmi Bodi ya mpya ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira (TUUWASA). Uzinduzi huo uliofanyika leo, uliendana na miongozo ya mamlaka za maji katika miji midogo na makao makuu ya wilaya, ambapo bodi hiyo inaundwa na wajumbe saba wenye dhamana ya kusimamia masuala ya maji na usafi wa mazingira katika wilaya hiyo.

Pichani (aliyesimama) ni Mkurugenzi TUUWASA Mhandisi.Cuthbert Richard Kiwia  

Uteuzi huu wa bodi mpya ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira umefanywa na Waziri mwenye dhamana katika serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb), utadumu kwa miaka mitatu  (3) kuanzia tarehe 12/02/2025 hadi tarehe 12/02/2028

Bodi hii itakayofanya kazi kwa miaka mitatu(3) inaundwa na Bwn. Jonathani A.Haule  ambaye ni Mwenyekiti na Mhandisi.Cuthbert Richard Kiwia ni Katibu, Wajumbe wakiwa ni Ndg.Chiza Cyprian Marando, Mhe.Hairu Hemedi Mussa, Bi.Fatuma A.Makumbusya, Bi.Marcela V.Mapunda na Adv.Kaukuya Yusuph Kaukuya.

Pichani ni Bwn. Jonathani A.Haule  ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi mpya ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira

Akizungumza katika hafla hiyo, Mheshimiwa Chacha aliwasisitiza wajumbe wa bodi hiyo kusimamia kwa umakini rasilimali za maji, miundombinu, na pia kufanya kazi kwa ushirikiano na mamlaka nyingine zilizopo ili kukabiliana na changamoto zozote zitakazojitokeza. Alikiri kuwa upatikanaji wa maji kwa sasa hautoshi kulingana na mahitaji ya wananchi, akisisitiza kuwa suala la maji linagusa uhai wa kila mmoja.

"Hali ya upatikanaji wa maji kwa sasa haitoshi kabisa ukilinganisha na mahitaji halisi, upo umuhimu wa usimamizi wa uwiano wa rasilimali za maji ili kuhakikisha kuwa maji hayawi kikwazo katika maendeleo ya jamii yetu " alizungumza Mhe. Chacha kwa msisitizo. "Tunapozungumzia suala la maji, tunagusa uhai wetu moja kwa moja, hivyo suala la kuendeleza na kusimamia rasilimali hii ili itumike katika kizazi cha sasa na cha baadae."

Aidha, Bodi hii mpya yenye jukumu kubwa la kuishauri serikali kupitia wizara ya maji namna bora ya kuboresha huduma ya bora ya maji katk mazingira yaliyopo inatarajiwa kuwa chachu katika kuhakikisha wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru wanapata huduma ya maji kwa ukamilifu. Mheshimiwa Chacha alimpongeza pia Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mjini Tunduru (TUUWASA) Mhandisi.Cuthbert Richard Kiwia  kwa kazi nzuri anayoifanya, akibainisha kuwa hakujakuwa na malalamiko yoyote hadi sasa, na mipango mipya kabambe ya kuboresha huduma inaendelea kuandaliwa kwa manufaa ya wananchi.

Hii ni bodi ya kwanza ya wakurugenzi kuundwa katika wilaya ya Tunduru kwa ajili ya mamlaka ya maji. Mheshimiwa Chacha aliongeza kwa kusema, "Wadau wa kwanza wa utumiaji wa maji ni wananchi wenyewe," alihimiza Mhe. Chacha. "Hakikisheni rasilimali maji zinatunzwa kwa kila hali. Ikiwezekana, undeni sheria ndogondogo ambazo zitawasaidia kuendesha bodi hii kwa ufanisi."

Uzinduzi huu unaashiria hatua muhimu katika jitihada za kuboresha huduma za maji na usafi wa mazingira kwa wakazi wa Tunduru, huku ushirikiano kati ya bodi, mamlaka zilizopo, na wananchi ukiwa ni nguzo muhimu ya mafanikio.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.