• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DCC TUNDURU YARIDHIA BAJETI 2026/27, YAUNGA MKONO MGAWANYO WA HALMASHAURI KUSOGEZA HUDUMA KWA WANANCHI

Imewekwa : February 16th, 2026



Tunduru, Februari 16, 2026

Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Tunduru (DCC), kilichoongozwa na Mhe.Denis Masanja, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, kimefanyika leo Februari 16, 2026 katika ukumbi wa Skyway, kwa lengo la kupitia na kujadili rasimu ya Mpango na Bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru kwa mwaka wa fedha 2026/2027.


Katika kikao hicho, wajumbe wa DCC walijadili kwa kina rasimu ya mpango na bajeti hiyo na hatimaye kuridhia kuipitisha, wakibainisha kuwa imezingatia vipaumbele vya maendeleo ya wananchi na mahitaji halisi ya Wilaya ya Tunduru.

Aidha, Kamati ilijadili na kuridhia mapendekezo ya kuigawa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru yenye ukubwa wa kilomita za mraba 18,778 kuwa Halmashauri mbili (2). Mchakato wa mgawanyo huo ulianza mwaka wa fedha 2018/2019, ukiwa na lengo kuu la kusogeza huduma karibu zaidi kwa wananchi, ikizingatiwa kuwa ukubwa wa eneo la kiutawala umekuwa changamoto katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa ufanisi na kwa wakati.


Kwa sasa, Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru inahudumia tarafa 7, kata 39, vijiji 157 na vitongoji 1,179. Wilaya hiyo pia ina majimbo mawili ya uchaguzi ambayo ni Tunduru Kusini, inayojumuisha tarafa 3 za Namasakata, Nalasi na Lukumbule, pamoja na Tunduru Kaskazini yenye tarafa 4 za Matemanga, Mlingoti, Nakapanya na Nampungu.

Umuhimu wa kuigawa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru unatokana na sababu kadhaa ikiwemo ukubwa mkubwa wa eneo la kiutawala na mtawanyiko wa kijiografia, idadi kubwa ya watu, kata na vijiji ikilinganishwa na Halmashauri nyingine, pamoja na haja ya kuwa na mgawanyo bora wa rasilimali fedha na rasilimali nyingine kulingana na idadi ya watu na ukubwa wa maeneo husika. Hatua hiyo inalenga kuimarisha utoaji wa huduma za kijamii, kuharakisha maendeleo ya wananchi na kuongeza ufanisi wa utendaji wa Serikali kwa ujumla.


Kikao hicho kilihitimishwa kwa wito kwa wadau wote kuendelea kushirikiana katika utekelezaji wa mipango na maamuzi yaliyofikiwa, kwa maslahi mapana ya maendeleo ya Wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • DCC TUNDURU YARIDHIA BAJETI 2026/27, YAUNGA MKONO MGAWANYO WA HALMASHAURI KUSOGEZA HUDUMA KWA WANANCHI

    February 16, 2026
  • DCC TUNDURU YARIDHIA BAJETI 2026/27, YAUNGA MKONO MGAWANYO WA HALMASHAURI KUSOGEZA HUDUMA KWA WANANCHI

    February 16, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI TUNDURU DC LAPITISHA RASIMU YA BAJETI YA SHILINGI BILIONI 55 KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027

    February 15, 2026
  • DAMU SALAMA, UHAI SALAMA: TUNDURU YAKUSANYA CHUPA 224 ZA DAMU KUPITIA SHULE ZA SEKONDARI

    February 06, 2026
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.