• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Video

  • SEQUIP yatatua utoro Sekondari za Tunduru

    August 23rd, 2023

    Afisa Elimu sekondari katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Mwl. Patrick Haule ameishukuru serikali ya awamu ya sita  kwa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa shule tano mpya kupitia programu ya uboreshaji wa Elimu Sekondari (SEQUIP).                        

    Akizungumza ofisini kwake mjini Tunduru Afisa Elimu sekondari katika Wilaya ya Tunduru Mwl. Patrick Haule amesema katika awamu ya kwanza ya utekelezaji wa SEQUIP kwa mwaka wa fedha 2022/2023 serikali ya awamu ya sita ilitoa zaidi ya shilingi bilioni 1.5 za ujenzi wa sekondari tatu mpya za kata ya Nakayaya, Majimaji na Lukumbule.

    Shule zote za awamu ya kwanza ya programu hii zimekamilika na zimechukuwa wanafunzi wa kidato cha kwanza zaidi ya 500 katika shule zote tatu kwa mwaka huu.

    Amesema kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Elimu Sekondari imepokea tena zaidi ya bilioni 1 kutoka serikali kupitia programu ya SEQUIP, ambapo shule mbili mpya toka kata ya Tinginya na Tuwemacho zitajengwa.

    “Wanafunzi walikuwa wakitembea umbali zaidi ya kilomita 15 hadi 20 kutoka kata moja kwenda kusoma kata nyingine, hali iliyokuwa ilipelekea kuwepo kwa utoro mkubwa ambao ulisababisha wanafunzi wengi kuacha shule.”Alisema

    Shule hizi za sekondari kupitia programu ya SEQUIP zitajengwa karibu na maeneo ya kuishi  ili kuwawezesha wanafunzi kufika shule kwa wakati.

    Imeandaliwa na Orpa Kijanda,Kaimu Mkuu Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

    23/08/2023.

  • MBAAZI zawaingizia wakulima Tunduru bilioni 1.6

    August 23rd, 2023

    WAKULIMA wa Mbaazi Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma wameingiza zaidi ya shilingi bilioni 1.69 baada ya kuuza Kilo 839,940 za mbaazi katika Mnada wa kwanza Msimu wa mwaka 2022/2023.

    Hayo yamesemwa na Meneja wa Oparesheni wa Chama Kikuu cha Ushirika Tunduru (TAMCU) Bw. Marcelino Mrope wakati akizungumza na Wanahabari ofisini kwake Mjini Tunduru.Bw, Mrope amesema TAMCU katika msimu wa Mwaka 2023/2024 imejiwekea malengo ya kukusanya Mbaazi Kilo 5,350,788 na kwamba katika msimu huu Chama kimeagiza viroba 130,000 kwa ajili ya kuhifadhia Mbaazi.

    Hata hivyo, amesema kuwa ukusanyaji wa Mbaazi katika msimu wa 2022/2023 uliendelea kuuzwa kwa mfumo wa Stakabadhi Ghalani, ambapo jumla ya Minada sita ilifanyika na Kilo 3, 035,692 ziliuzwa na kuwaingizia Wakulima zaidi shilingi bilioni 2.6.

    “ukusanyaji wa zao la Mbaazi umepungua kidogo kutoka kilo 4,111,845 msimu wa mwaka 2021/2022 hadi kilo 3,035,692 msimu wa mwaka 2022/2023 ambapo ni sawa na anguko la asilimia 26.17 la ukusanyaji katika mauzo”, alisema.

    Mnada wa pili wa zao la Mbaazi Wilayani Tunduru unatarajia kufanyika katika kijiji cha Msinji Agosti 24, 20

    Imeandaliwa na Orpa Kijanda,Kaimu Mkuu Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

  • BILIONI 1.2 kuboresha miundombinu ya afya Tunduru

    August 22nd, 2023

    BILIONI 1.2 KUBORESHA MIUNDOMBINU YA AFYA TUNDURU

    Serikali ya awamu ya sita imetoa bilioni 1.2 kuboresha miundombinu ya hospitali kongwe iliyoanzishwa mwaka 1930 wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma.

    Mganga mfawidhi wa hospital ya wilaya ya Tunduru, Daktari Athumani Mkonoumo amesema wamepokea shilingi milioni 900 kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya hospitali hiyo ambayo inajenga maabara mpya, Jengo la wagonjwa wa nje (OPD) na chumba cha upasuaji.

    Amesema Serikali pia imetoa shilingi milioni 300 kwa ajili ya ujenzi wa Jengo ya wagonjwa wa Dharura (EMD), na kwamba limekamilika na kuanza kutoa huduma za dharura tangu Juni mwaka huu.

    Vilevile, hospitali imepokea vifaa vya matibabu katika jengo hilo la dharura (EMD), vifaa hivi ni pamoja na Mashine ya X-Ray, Utrasound na mashine za kusaidia kupumua pamoja mitungi ya gesi ambapo hadi sasa wagonjwa zaidi ya 86 wamefanikiwa kupatiwa huduma zinazotolewa na EMD.

    “Itatusaidia sana kutoa huduma bora na stahiki kwa sababu hatutokua na changamoto kubwa ya vifaa na miundombinu sahihi ya kutoa hizo huduma”. Alisema.

    Ukarabati huu mkubwa wa hospitali utapunguza idadi kubwa ya wagonjwa kupewa rufaa ya kwenda kupata huduma nje ya wilaya.

    Imeandaliwa na Orpa Kijanda,Kaimu Mkuu Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

    22/08/2023.

  • ← Prev
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • Next →

Matangazo

  • No records found
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • COUNSENUTH yahitimisha mradi wa Kijana Jiongeze awamu ya pili.

    August 15, 2024
  • “TOENI taarifa zinazohusu vitendo au viashiria vya rushwa na ukiukwaji wa Sheria, taratibu na kanuni za Uchaguzi”-Bwana George Njogolo, Mkuu wa TAKUKURU Tunduru

    August 13, 2024
  • MWENYEKITI CCM TUNDURU ATEMBELEA BANDA LA HALMASHAURI.

    August 06, 2024
  • MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA TUNDURU MHESHIMIWA HAIRU MUSA NDANI YA MAONESHO YA NANENANE MBEYA.

    August 06, 2024
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

Tovuti linganifu

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.