• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

ZIARA ya Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe. Simon Chacha kusikiliza na Kutatua kero za wananchi.

Imewekwa : July 4th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mheshimiwa Simon Chacha amefanya mkutano wa hadhara na wananchi wa kijiji cha Misechela na kata ya Namasakata. Lengo la mkutano huo lilikuwa kusikiliza kero za wananchi na kutatua.

Katika mkutano huo, Mkuu wa Wilaya alionya wafugaji holela wanaokaidi agizo la kupeleka mifugo yao kwenye vitalu vilivyotengwa. Aliwaagiza waache kupeleka mifugo yao kwenye mashamba ya wakulima na badala yake wafuate sheria kwa kuweka mifugo yao kwenye vitalu.


Mhe. Chacha pia aliwaasa wakulima na wafugaji kukaa pamoja na kutafuta suluhisho la changamoto zao kwa amani badala ya migogoro. Alisema kuwa ana jukumu la kuhakikisha usalama wa wananchi wote wa Tunduru, lakini akaomba ushirikiano kutoka kwa jamii ili kuishi kwa amani na utulivu.

Pichani ni Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe. Simon Chacha akizungumza na wananchi.

Mbali na hilo, Mhe. Chacha alisisitiza pia juu ya ulinzi wa watu wenye ulemavu wa ngozi. Aliagiza kutokuruhusu kufanyiwa vitendo vya ukatili, na akasema, "ninaomba tuwalinde watoto hawa kwa umoja wetu. Jamii inayomzunguka ndio mlezi wa kwanza. Tutambue kuwa wana haki zote za kibinadamu. Msiwafanyie vitendo vya kikatili wala kuwaficha ndani. Toeni taarifa ili tuhakikishe wanapata ulinzi."

Kwa upande wake, Mkuu wa Jeshi la Polisi wilaya ya Tunduru, SSP.Shadrack Msasa, alieleza kuwa tayari wameanza kukusanya taarifa za watoto wenye ulemavu wa ngozi wote waliopo katika Wilaya ya Tunduru. Aliwaagiza Watendaji na wenyeviti wa vijiji zote kushirikiana katika kukamilisha orodha ya watoto hawa na kuwaweka kwenye kanzidata kwa ajili ya ulinzi bora zaidi.

Pichani ni Mkuu wa Jeshi la Polisi wilaya ya Tunduru, SSP.Shadrack Msasa

Mkutano huo ulifanyika kwa amani na utulivu, na wananchi walionyesha shukrani kwa Mkuu wa Wilaya ambaye pia alijitambulisha kwao, kusikiliza kero zao na kuzitatua.

Imetolewa na Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru,

Orpa Kijanda,

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.