• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WILAYA YA TUNDURU YAPATIWA DAWA ZA KUKINGA MAGONJWA YALIYOKUWA HAYAPEWI KIPAUMBELE

Imewekwa : February 23rd, 2024

WILAYA YA TUNDURU YAPATIWA DAWA ZA KUKINGA MAGONJWA YALIYOKUWA HAYAPEWI KIPAUMBELE

Wilaya ya Tunduru imepokea dawa za kukinga Magonjwa mbalimbali yaliyokuwa hayapewi kipaumbele (NTDs), ambapo zoezi la Ugawaji Ngazi ya jamii linatarajiwa kuanza February 23, 2024.

Hayo yamesemwa na Mratibu wa zoezi la ugawaji dawa hizo za kinga, Ndg. Baraka Mmari, katika mafunzo ya jinsi ya ugawaji dawa  katika ngazi ya jamii, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Hospitali ya Wilaya ya Tunduru.

Alisema, Zaidi ya watu 400,000 watapatiwa dawa kinga dhidi ya magonjwa haya katika vijiji vyote 157 vilivyopo katika Wilaya ya Tunduru, ambapo zaidi ya Milioni 200 zitatumika kukamilisha zoezi hilo.

Ndg. Mmari aliwataka watoa huduma ya ugawaji dawa kwenda kutoa elimu Kwa jamii kuhusu namna bora ya kujikinga na Magonjwa haya. Alisema kuwa elimu ni muhimu sana kwa sababu itasaidia jamii kuelewa umuhimu wa kutumia dawa za kinga na jinsi ya kuzitumia kwa usahihi.

Aidha, Aliwasisitiza watoa huduma hao, kuhakikisha wanatembelea kila kaya na kutoa Huduma hiyo, pia kuhakikisha kila Mwananchi anapatiwa huduma hiyo ya dawa kinga za Magonjwa hayo.

“Tunaamini bila ninyi zoezi hili haliwezi kukamilika, tunaomba tuoneshe uzalendo katika kufanya hili zoezi ili tuzidi kuimalisha afya katika Wilaya yetu”. Alisema Mmari.

 Mmari alitoa taaria ya Baadhi ya magonjwa yaliokuwa hayapewi kipaumbele yanayoathiri Wilaya hii ni pamoja na usubi, Kichocho, ugonjwa wa minyoo, ugonjwa wa Matende na Mabusha

Aidha, Bw. Mmari alitoa wito kwa Wananchi kuonesha ushirikiano kwa watoa huduma hao pale tu wanapofika katika makazi yao, kwani zoezi hili linakwenda kuimarisha afya zetu katika jamii.

Mafunzo haya yalihudhuriwa na watoa huduma ya ugawaji dawa hizo kutoka katika ngazi ya Jamii kutoka katika Vitongoji vyote vilivyopo Wilaya ya Tunduru . Ambapo Watoa huduma hawa watawajibika kwa ugawaji wa dawa za kinga kwa jamii katika Vitongoji vyao katika kila kaya.

Baadhi ya Watoa huduma za kugawa Dawa kinga wakitoa maoni kuhusu Magonjwa yaliyokuwa hayakupewa kipaumbele.

Mratibu wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.