• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

watendaji waagizwa kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia majukumu yao

Imewekwa : August 1st, 2019

Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Tunduru Mhe.Julius Mtatiro wakati akiongea na watumishi wa Idara ya Mifugo na Kilimo,watendaji wa Kata pamoja na maafisa Tarafa katika kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa klasta mapema wiki hii cha kutatua migogoro ya wakulima na wafugaji wilayani Tunduru.

Akiongea katika ufunguzi wa kikao hicho Mhe.Julius Mtatiro alianza kwa kuwapongeza watendaji kwa utendaji kazi uliotukuka wa  kuleta mabadiliko makubwa ya kiuchumi na kijamii katika wilaya ya Tunduru ikiwa ni pamoja na kufunguka kwa barabara ya lami na kurahisha usafirishaji na uchukuzi.

Mkuu wa wilaya huyo alisema anapenda kufanya kazi na watu wanatoa taarifa zilizo sahihi na mashauriano “nendeni  mkasome mjue majukumu yenu ni yapi usisubiri mpaka kuagizwa na mkuu wa idara yako ya kilimo au mifugo, siamini katika falsafa ya kuletewa taarifa ndio utekeleze majukumu yako”

Aidha katika kikao hicho aliweka mikakati ya utendaji kazi ambayo itaenda kutatua migogoro iliyopo kati ya wakulima na wafugaji, ikiwa ni pamona na mikataba ya vitalu kwenye maeneo tengefu iwe shirikishi kwa Maafisa Tarafa na Watendaji wa kata ili kuwa na nguvu ya kufanya maamuzi inapotokea hali ya kutokuelewana kati ya wakulima na wafugaji.

Maafisa kilimo na mifugo wa Kata waache kufanya kazi kwa mazoea, wengi wao wanasubiri kuagizwa na wakuu wa wao wa idara, aliwataka kuamka na kutafuta taarifa na kuwahudumia wananchi kwenye maeneo waliyopangiwa.

Halmashauri kupitia baraza la madiwani kutunga sheria ndogo mahusuano kwa ajili ya usimamizi wa mifugo ili itumike katika kupunguza migogoro, pia kuhuisha sheria ndogo za Halmshauri ambayo itatoa mwelekeo wa uendeshaji wa shughuli za wafugaji na wakulima katika hali ya Amani na usalama.

Serikali ipo katika hatua za kuhakikisha kuwa maeneo yote tengefu ya vitalu vya wafugaji miundombinu wezeshi inajengwa ili kupunguza ufugaji wa kuhamahama kutoka sehemu moja hadi nyingi kutafuta malisho hasa wakati wa kiangazi.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Tunduru Ndg Gasper Balyomi alipokea maelekezo hayo na kuwataka watendaji wote na maafisa waliopo katika ngazi ya kata kuwa makini na kushughulikia masuala yanayohusu migogoro ya wakulima na wafugaji kwani yanaweza kuleta maafa makubwa kwa jamii ya Tunduru.

Aidha aliwataka kuhakikisha kuwa wafugaji wanatekeleza masharti waliyopewa wakati wanapangiwa vitalu na endapo watakua wanakiuka utaratibu na sheria iliyowekwa basi wapigwe faini kulingana na sheria ya mazingira ya mwaka 2004, na ikifanyika hivyo wafugaji wataacha kuvunja sheria.

Vilevile alikema tabia ya watendaji kuruhusu wakulima na wafugaji kumaliza migogoro kienyeji iachwe mara moja na ifike mwisho kwani ndio linalochochea migogoro kuendelea kuwepo “suala la wakulima na wafugaji kumalizana kienyeji lifike mwisho, sheria izingatiwe, hii kuelewana iishe, mtu akifanya kosa apigwe faini kubwa”

Kwa upande wa kamanda wa polisi wilaya Livingstone Nicholausi Mwakasanga alikemea tabia ya baadhi ya viongozi wa kisiasa kuhamasisha migogoro ya wakulima na wafugaji, akitaja baadhi ya maeneo ya sisi kwa sisi, kijiji cha Angalia, na Mwenge imechangiwa kwa kiwango kikubwa na viongozi.

Hata hivyo waliaswa kuacha tabia ya kupenda kupokea zawadi ndogondogo ambazo zinawapelekea kushindwa kutekeleza majukumu yao.

Mwisho.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.