• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Watendaji wa Kata wasaini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe

Imewekwa : July 29th, 2019

Zoezi la usainishaji wa mikataba ya utekelezaji wa afua za lishe ngazi ya Kata na kijiji limenguliwa na mkuu wa wilaya ya tunduru Julius S mtatito, ukiwa na lengo la kuboresha hali ya lishe na kuondoa athari za utapiamlo katika jamii, na kufanya suala la lishe kuwa ajenda kuu ya kudumu katika mabaraza ya maendeleo ya Kata.

Akiongea na watendaji wa Kata wakati wa kusaini mkataba wa utekelezaji wa afua za lishe ngazi ya Kata mkuu wa wilaya  ya Tunduru Julius S. Mtatiro alisema masuala ya lishe ni mapana sana ambayo yanahusisha sekta mbalimbali kama kilimo, Mifugo, Afya, Maji.

Masuala ya lishe sio jambo la kitabibu pekee ni jambo la kijamii na wilaya  imeanza kuchukua hatua ya kutokomeza udumavu, ukondefu, uzito pungufu na  upungufu wa vitamin kwenye makundi maalum.

watendaji wa Kata wakifuatilia kwa makini maagizo ya mkuu wa wilaya Julius Mtatiro 

Mkuu wa wilaya huyo aliwataka watendaji Kata kutumia nafasi zao katika jamii kuhakikisha suala la lishe linakuwa ni ajenda ya kudumu katika vikao vya maendeleo ya Kata, “ninataka watendaji wote wa kata mwende mkatumie nafasi zenu kwa kuwa nyie ndio injini ya utekelezaji wa kazi, nitaanza kukagua mihtasari ya vikao vya mabara ya kata kuona kama suala la lishe limekua ajenda ya kudumu katika vikao vyenu kuona kama lishe imekua ajanda kwenye vikao vitakavyofanyika kanzia sasa” alisema Mkuu wa wilaya Julius Mtatiro.

Aliendelea kutabaisha kuwa lishe ni msingi na uti wa mgongo wa uhai wa mwanadamu na lishe ni kitu ambacho hakikwepeki, kila kata iende kutengeneza mpango kazi wa utekelezaji wa afua za lishe katika Kata na Vijiji na kusimamia.

Akitoa mfano wa aina ya watendaji katika mikoa 12 aliyotembelea mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa serikali ina watendaji Kata wenye ueledi mkubwa sana, zaidi ya asilimia 70 ni wazuri lakini wengi wao wanakwepa kutekeleza majukumu yao kwa visingizio tofauti  visivyokua na tija.

Aidha alisema utekelezaji wa afua za lishe unaenda sambamba na usafi wa mazingira, mazingira safi kwa maeneo ya kutoa huduma hasa za chakula, “opesheni ifanye katika maeneo yanayotoa huduma za chakula, kila mtendaji akatoe elimu kwa wananchi kabla ya kuwakata, utolewe muda ili kama hawajatekeleza ndio hatua zifuate.

Hata hivyo alimuagiza Mkurugenzi Mtendaji kupitia baraza la madiwani kutunga sheria ndogo itakayosimamia utekelezaji wa afua za lishe itakayowabana wananchi, tukitunga sheria ndogo iatasaidia jamii kushiriki moja kwa moja katika kuondoa tatizo la udumavu ndani ya wilaya ya Tunduru.

Naye afisa lishe wilaya Bi Martha Kibona amesema mikata hii hii inalenga katika kuboresha hali ya lishe na kuondo tatizo la udumavu na utapiamlo kwani watendaji wa kata ndio viongozi ambao wataenda kusimamia utelekezaji wa afua za lishe na kufikia malengo yaliyowekwa na serikali kuwa na jamii isiyokuwa na udumavu, uzito pungufu, utapiamlo na ukondefu ifikapo 2021.

Mwisho.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • HARAMBEE YA UJENZI WA OFISI YA CCM TUNDURU YAKUSANYA ZAIDI YA MILIONI 106 PAMOJA NA MIFUKO 15 YA SARUJI.

    December 29, 2025
  • MHESHIMIWA SEFU HASSAN DAUDA NDIYE MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA TUNDURU

    December 05, 2025
  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.