• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Warsha -Stakabadhi Ghalani

Imewekwa : March 9th, 2018

Benki ya NMB Tunduru kwa kushirikiana na mamlaka ya Mapato Tanzania TRA tawi la Tunduru na Bodi ya korosho wamefanya warsha ya kujadili changamoto zilizojitokeza  katika uuzaji wa zao la korosho wilayani Tunduru katika mfumo wa stakabadhi ghalani katika msimu wa mwaka wa 2017/2018 ambapo malipo yalifanywa kwa njia ya Benki tofauti na miaka ya nyuma ilivyokuwa wakulima kulipwa fedha zao mikononi.

Warsha hiyo ilihudhuriwa na viongozi wa vyama vya msingi vya ushirika, viongozi wa serikali, chama kikuu cha ushirika Tunduru (TAMCU), wawakilishi wa Bodi ya korosho, meneja wa  mamlaka ya mapato Tanzania tawi la Tunduru na menejenti ya benki ya NMB kanda ya kusini ambao ndio waandaji wa warsha hiyo.

Akizungumza katika warsha hiyo kaimu meneja kanda ya kusini Bi.  Janeth Shango aliwashukuru wananchi wa wilaya ya Tunduru kwa kuchagua benki ya NMB kupisha malipo ya  fedha zao kwani zitokanazo na zao la korosho, kwani ni zaidi ya shilingi bilioni 79 zimetishwa katika benki ya NMB tawi la Tunduru.

Meneja wa Benki Tawi la NMB Tunduru  Ndg Goodluck Shirima akitoa elimu ya mikopo kwa wakulima katika warsha iliyofanyika katika ukumbi wa klasta ya Mlingoti ya kujadili changamoto zilizojitokeza katika uuzaji wa zao la korosho wilayani Tunduru katika msimu wa mwaka 2017/2018

Meneja wa NMB kanda ya Kusini Bi shango alisema kuwa changamoto kubwa iliyojotokeza katika ulipaji wa fedha za wakulima katika msimu huu ni kukosemna kwa uaminifu miongoni mwa wakulima waliokuwa wanatumia akaunti moja kuchulipwa kwani walijitokeza waliodai malipo mara mbili wakati wameshalipwa tayari.

Vilevile taarifa za kibenki kwa baadhi ya wakulima kutofautina na zile zilizopo katika vyma vya msingi hivyo kuleta usumbufu mkubwa sana, alisema unakuta mkulima anaitwa Juma saidi Issa lakini jina la akaunti Benki ni Saidi Issa.


Naye mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Zuberi Homera aliviagiza vyama vyote vya msingi vya Ushirika wilayani Tunduru ambavyo bado hawajalipa fedha za wakulima kufanya malipo hayo ndani ya muda wa wiki moja tofauti ya hapo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Picha ya pamoja ya viongozi wa viongozi wa vyama vya msingi na menejementi ya benki ya NMB Kanda ya kusini baada ya  warsha ya majadiliano ya changamoto  zilizojitokeza katika msimu wa mwaka 2017/2018 na njia za kuzitatua katika msimu ujao wa mauzo ya zao la korosho wilayani Tunduru.

"naagiza wakulima wote ndani ya wiki moja wawe wamelipwa fedha zao za mauzo ya korosho ya msimu 2017/2018, kwa chama chochote kitakachokiuka maagizo hayo viongozi wake kuanzia mwenyekiti, na viongozi wa ngazi ya chini yake  watachukuliwa hatua za kisheria"alisema mkuu wa wilaya Tunduru Juma Homera.

Juma Homera alitanabaisha kwamba ni vyema kwa benki ya NMB kusogeza huduma zake kila Tarafa kwa kufungua matawi na kuongeza vituo vya ATM (mashine za kutolewa fedha) pamoja kuanzisha (NMB mobile car) na kuboresha huduma za kibenki kupitia simu (NMB mobile) ili kupunguza msongamano kwenye benki iliyopo.

Meneja wa Mamlaka ya mapato Tanzania tawi la Tunduru Ndg Joshua Mwakatumbula akitoa elimu ya mlipa kodi katika warsha hivi leo wakati wa majadiliano


Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.