• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Warajisi wasaidizi na Maafisa Ushirika Wilaya Simamieni ushirika.

Imewekwa : May 24th, 2018


“Warajisi Wasaidizi wa Mikoa na Maafisa Ushirika wa Halmashauri za Wilaya nchini wakutane na wadau wa vyama vya msingi vya zao la kahawa na wapitie upya tozo zilizo kwenye zao hilo, hayo ameyasema Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Kassimu Majaliwa  katika ukumbi wa hazina jijini Dodoma”.

Aliyasema hayo wiki iliyopita  (Jumamosi, Mei 19, 2018) wakati akizungumza na Warajisi Wasaidizi wa Ushirika wa Mikoa 25 na Maafisa Ushirika wa Halmashauri za Wilaya 140 zinazolima mazao makuu ya biashara yaani kahawa, chai, tumbaku, pamba na Korosho kwenye kikao alichokiitisha jijini Dodoma ili kujadili namna bora ya kuongeza uzalishaji wa mazao hayo na kufanya ufuatiliaji wa maagizo ambayo alikwishayatoa kwenye ziara zake mikoani.

Alisema tozo nyingi haziko kisheria bali zinawekwa na vyama vya msingi na zimelenga kuwanyonya wakulima badala ya kuwasaidia kuinua vipato vyao.

 Akizungumzia kero ya tozo za mazao kwa wakulima, Waziri Mkuu alisema: “Kuna tozo nyingi zinazowekwa na vyama vya msingi na hazina uhalali wowote; tozo nyingine si za vyama vikuu, bali ni za AMCOS tu (vyama vya msingi)”

Akitoa mfano Waziri Mkuu alisema, “Wakati napitia nakala za baadhi ya vyama vya zao la kahawa, nimekuta chama kimoja cha Karagwe kimeweka sh. bilioni tano zikiwa ni gharama za kukagua maghala na ili kufidia gharama hizi, mkulima anakatwa sh. 260 kwa kilo moja. Nimejumlisha makato ya tozo zote nimepata sh.1,600 kwa kilo.”

Aidha waziri mkuu aliwataka warajisi pamoja na maafisa ushirika wilaya kufanya usimamizi wa mifumo ya masoko ili kupambana na wanunuzi nje ya mifumo iliyokusudiwa na serikali na kuwaibia wananchi.

 “Kuna mifano ya wanunuzi wasio rasmi katika mkoa wa Kagera wanunuzi wa kahawa wasio rasmi wanaitwa butura, Moshi wanaitwa katakichwa, kwenye korosho wanaitwa kangomba na kwenye tumbaku wanaitwa vishada. Ninawasihi msikubali kuwe na uonevu, dhuluma na wizi kwa wakulima wetu,” alisisitiza.

Waziri mkuu aliwataka maafisa hao kuhakikisha kuwa wana  takwimu sahihi ambazo zitaonesha idadi ya vyama vya msingi na wanachama wake, na kila mkulima analima ekari ngapi kwa msimu  ili kusaidia na kurahisha usambazaji wa pembejeo za kilimo.

Aliendelea kutanabaisha kuwa serikali imeamua kuanza kuimarisha  mazao manne ya biashara ili kuhakikisha kuwa wakulima wananufaika kwa kupata matunda ya kazi zao, mazao hayo ni pamoja  na Kahawa, Pamba, Chai,Korosho na Tumbaku.

 Naye Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini, Dk. Titus Kamani aliwataka maafisa hao wawe wabunifu na waondokane na utendaji wa mazoea ili wawasaidie wananchi kwa sababu ushirika ni silaha ya wanyonge na adui wa matajiri wanaowanyonya wakulima.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.