• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Wanawake tumieni fursa ya Mikopo kujiendeleza Kiuchumi.

Imewekwa : March 11th, 2020

Hayo yamesemwa na mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Tunduru Ndg.Gasper Zahoro Balyomi kabla ya kukabidhi hundi ya 103,112,284.00 ikiwa ni awamu ya tatu utekelezaji wa utoaji wa mkopo wa kisheria wa asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa vikundi 37 vya wanawake 14, vijana 14  na watu wenye ulemavu vikundi 9.

Halmashauri inaendelea kuwawezesha wanawake ili kuweza kujiinua kiuchumi na itawasimamia katika kuhakikisha kuwa mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu inakuwa endelevu kwa kipindi chote  atakachokuwa akitoa huduma katika halmashauri ya Tunduru,.

Naahidi kuendelea kuwaendeleza wanwake kiuchumi kwa kuwashika mikono kwa kutoa mikopo ya asilimia kumi katika mapato ya ndani, amesema "mimi kama mkurugenzi kupitia idara ya maendeleo ya jamii nitaendelea kuwainua wanawake kwa kuwa nimeona mnaweza na pia kupitia idara ya sheria nitahakikisha wanafika hadi vijijini na ile mifumo dume yote inayokandamiza wanawake inaondolewa kabisa"

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Tunduru Ndg.Gasper Balyomi (Kulia) akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani Milioni 103.1 kwa kaimu Mkuu wa wilaya ya Tunduru ambaye pia ni katibu tawala wilaya Ndg.Ghaibu Lingo wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika katika uwanja wa baraza la iddi.

Akiongea katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani kaimu mkuu wa wilaya ya Tunduru Ndg.Ghaibu Lingo baada ya kukabidhiwa Hundi na mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Tunduru kwa ajili ya kukabidhi kwa vikundi 37 aliwataka wanufaika wa mkopo huo kuutumia katika kujiletea maendeleo na sio kwenda kufanya shughuli ambazo ziko nje ya mpango kazi walioombewa ili kujikwamua kiuchumi na kutoa nafasi kwa vikundi vinginge kuweza kukopeshwa zaidi.

Aidha aliendelea kusema kuwa mkopo huo sio zawadi inayotolewa kwao bali wanatakiwa kurejesha kwa wakati ili kuongeza wigo wa utoaji mkopo kwa vikundi vingine vingi zaidi na kukuza uchumi wa wananchi kwa vikukndi na mtu mmoja mmoja.

Kimu mkuu wa wilaya ya Tunduru Ndg.Ghaibu Lingo akitoa maekelezo ya serikali kwa vikundi 37 vya walemavu, wanawake na vijana vilivyopatiwa mkopo na halmashauri katika siku ya wanawake duniani.

Pamoja na hayo Ndg.Ghaibu Lingo aliwataka wanawake kupendana na kutumia nafasi za uongozi walizonazo katika kuwainua wanawake wengine lakini pia kujitokeza katika uchaguzi mkuu wa mwezi octoba 2020 ili kupingana na dhana potofu ya kugombea katika nafasi za viti maalum "twende tukagombee majimbo na sio kusubiria nafasi za kuteuliwa za viti maalum pekee kwani wanawake tukiungana tunaweza"

Nao wanufaika wa mkopo huo wa milioni 103.1 waliishikuru serikali ya Halmashauri ya wilaya ya Tunduru kuendelea kuwashika mkono katika kuwakopesha mkopo usiokuwa na riba kwani umewatelea manufaa makubwa sana hadi kufikia sasa wengi wao wanamiliki biashara, kufuga kwa tija na vipato vya familia zao vimeongezeka ukilinganisha na awali ambapo hawakupata mkopo kutoka serikalini.




Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.