• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

“WANAFUNZI wote waliofauru wawe wameandikishwa shuleni ifikapo tarehe 12 mwezi huu” Mhe.DC Mtatiro

Imewekwa : January 5th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mh. Wakili Julius S. Mtatiro, amefanya kikao kazi na watendaji Kata, waratibu wa Elimu Kata pamoja na Magavana katika maandilizi ya kupokea wanafunzi mwaka wa masomo 2024. Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa Klasta- Mlingoti tarehe 05.01.2024.

Pichani ni Watendaji Kata, waratibu wa Elimu Kata pamoja na Magavana wakiwa katika kikao kazi.

Katika kikao hicho Mh. Wakili Mtatiro aliwapongeza watendaji hao kwa kazi wanayoifanya katika kata zao, ya kuhakikisha suala la Elimu linapewa kipaumbele. Aliwataka waendelee kufanya kazi kwa bidi ili kuhakikisha wanafunzi wote wanaohitimu elimu ya msingi wanapata fursa ya kujiunga na Elimu ya Sekondari.

Mh. Wakili Mtatiro aliagiza kuhakikisha wanakutana na wazazi/walezi wote ambao watoto wao wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza ndani ya siku tatu ambazo ni kuanzia  tarehe 06-07 mwezi Januari 2024. Pia, aliwataka magavana kupeleleka taarifa ya idadi ya wanafunzi wote waliofauru kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka huu ifikapo siku ya jumanne, tarehe 09 Januari 2024.

“Vikosi kazi na Polisi kata wote waende kwenye kata zao, ili washiriki kikamilifu kwenye vikao vya wazazi na viongozi wa kata” Alisema Mh. Wakili Mtatiro “Miundombinu tumeikamilisha hivyo, ni wajibu wetu kusimamia na kuhakikisha vijana wanapata Elimu”

Aidha, Mh. Wakili Mtatiro alisisitiza kuwa zoezi hili linawapasa viongozi wote kuanzia ngazi ya kijiji, kata pamoja na magavana kushiriki kikamilifu, pia, aliagiza kuwa wazazi/walezi wote wataokaidi kupeleka wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka wa masomo 2024, kukamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sharia haraka.

Akifunga kikao hicho Mh. Wakili Mtatiro alisisitiza kuwa Elimu ni haki ya kila mtoto, hivyo ni wajibu wa mzazi/mlezi kuwapeleka watoto wao shule. Aliwataka watendaji wote wanaosimamia sekta ya Elimu Wilayani Tunduru kuhakikisha wanasimamia na kutekeleza yale yote ambayo Wizara na Serikali imeyawekea mikakati ili kuboresha Elimu nchini Tanzania. Alionya kuwa hakuna atakayeruhusiwa kukwepa wajibu huu.

Shule zote Wilayani Tunduru zinatarajiwa kufunguliwa na kuanza kupokea wanafunzi ifikapo Jumatatu ya tarehe 08 Januari mwaka 2024, hivyo wawazi/walezi wote wanaagizwa kupeleka wanafunzi wao ili wakaandikishwe kujiunga na elimu msingi na awali pamoja na Elimu ya Sekondari.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.