• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WANAFUNZI 1,874 Kupata Fursa Vyuo vya Ufundi Tunduru.

Imewekwa : February 28th, 2024

WANAFUNZI 1874 , kupata fursa vyuo  ufundi Tunduru

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mhe. Wakili, Julius S. Mtatiro, amewakabidhi Wakuu wa vyuo vya ufundi Wilayani humo majina ya Wanafunzi ambao wanakosa sifa za kujiunga na kidato cha kwanza, cha tano na vyuo vya kati kwa mwaka 2024.

Makabidhiano hayo yamefanyika katika kikao kazi kilichofanyika katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, ambapo kilihudhuriwa na Maafisa Elimu Msingi, Elimu Sekondari na Wakuu wa vyuo vya Ufundi Nandembo (FDC) ,Mbesa na Kiuma.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Maafisa wa Elimu ya Sekondari na Elimu ya Msingi wamesema majina 1,874 yamekabidhiwa, ambapo Wanafunzi 1,326 ni wa elimu ya sekondari na Wanafunzi 548 ni wa elimu ya msingi.

Hatua hii imefikia baada ya  Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe. Wakili Julius S. Mtatiro kuwataka Idara ya Elimu Msingi na Sekondari kutambua majina ya wanafunzi hao waliokosa sifa ya kujiunga na elimu ya kidato cha kwanza, kidato cha tano na vyuo vya kati kwa Mwaka 2024.

Ambapo hapo awali, alizungumza na wakuu wa vyuo hivyo kuweza kuwapatia nafasi kwa Wanafunzi hao ambao wanakosa sifa hasa za kujiunga na Elimu inayofata hasa kidato cha kwanza, kidato cha tano na Vyuo vya kati.

Akizungumza kabla ya makabidhiano hayo, Dc, Mtatiro amewasisitiza wakuu wa vyuo hivyo kuyafanyia kazi majina hayo na kuandaa fomu za kujiunga na vyuo hivyo ili kuwawezesha Wanafunzi hao kuripoti mapema iwezekanavyo na kuanza masomo yao.

“Jambo hili linakwenda kuwa msaada mkubwa  katika kumaliza tatizo la watoto wetu kukosa fursa”. Alisema Dc, Mtatiro “ kwani itakuwa nyenzo kubwa ya kutatua tatizo la ajira na vijana kuweza kujiajiri”.

Wakuu wa vyuo vya ufundi wamesema kwa nyakati tofauti kuwa, wako tayari kushirikiana kwa ukaribu  katika kuwapokea katika vyuo vyao.

Hatua hii inatarajiwa kusaidia wanafunzi ambao hawakupata fursa ya kujiunga na elimu ya juu kupata elimu ya ufundi na kujiajiri.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.