• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WAKUTWA NA SILAHA YA KIVITA,MENO YA TEMBO

Imewekwa : July 18th, 2019





JESHI la Polisi mkoani Ruvuma, linawashikilia watu watano wa Kijiji cha Magwamila Songea Vijijini  kwa kosa la kumiliki Silaha ya kivita aina ya AK 47.

Akizungumza na Waandishi wa Habari ofisini kwake jana,Kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma Simon Maigwa alisema, tukio hilo lilitokea taerehe 15 mwezi huu huko mto Ruvuma.

Kwa mujibu wa kamanda Maigwa, Fidel Mangala(20) alikutwa na silaha  hiyo na katika mahojiano ya kina aliwataja wenzake ambao anashilikiana nao katika  kufanya uharifu katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Ruvuma na Nchi jirani ya Msumbuji.

Kamanda Maigwa aliwataja watuhumiwa wengine ni Maulid Jafar(45) mkazi wa Kijiji cha Nambendo, Maganga Msoma mkazi wa Nambedo na Shame Omari(45)mkazi wa Nchi jirani ya Msumbiji ambaye yupo Magereza  kwa kosa la kupatikana na silaha nyingine ya kivita aina ya AK 47.

Aidha kamanda Maigwa alisema, baada ya mahojiano  ya kina watuhumiwa hao waliongoza hadi eneo walikoficha silaha hiyo ambayo walifukia Ardhini na baada ya kufukua eneo hilo ilipatikana silaha moja ya kivita aina ya AK 47 pamoja na risasi sita ndani ya magazine.

Kamanda huyo wa polisi alieleza kuwa, watuhumiwa hao wote walikiri kujihusisha na uwindaji haramu na matukio mengine ya uharifu ndani ya Tanzania na Nchini Msumbiji kwa muda mrefu.

Hata hivyo Kamanda Maigwa alisema, katika kufuatilia mtandao wao wa ujangili pia walifanikiwa kuwakamata watu wawili Issa Millanzi(46) na Fidel Mangala(20)wakazi wa Kijiji cha Nambendo Songea vijijini wakiwa na meno mawili ya Tembo yenye thamani ya shilingi Ml34.5 ambayo waliyahifadhi kwenye mfuko wa Sulphate na kuyafikia ardhini katika shamba la Issa Musa.

Kamanda Maigwa aliwaeleza waandishi wa Habari kuwa,watuhumiwa hao walikiri kuwa silaha hizo ndizo walitumia kuulia tembo na kupata meno  hayo.

Amewataka wakazi wa mkoa wa Ruvuma kwa wale wanaomiliki silaha kinyume na sharia wazisalimishe haraka iwezekanavyo na kuwataka waache kujihusisha na uwindaji haramu n ahata matukio ya kiharifu kwani Jeshi la Polisi limejipanga kikamiifu na halitasita kuwakamata na kuwachukulia hatua wale wote wanaojihusisha na matukio ya uharifu.
MWISHO















ReplyReply allForward






Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • HARAMBEE YA UJENZI WA OFISI YA CCM TUNDURU YAKUSANYA ZAIDI YA MILIONI 106 PAMOJA NA MIFUKO 15 YA SARUJI.

    December 29, 2025
  • MHESHIMIWA SEFU HASSAN DAUDA NDIYE MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA TUNDURU

    December 05, 2025
  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.