• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

wakulima wa ufuta Tunduru wapata bilioni 1.4.

Imewekwa : June 4th, 2019

Wakulima wa ufuta wilayani Tunduru wameipongeza serikali kwa kusimamia soko la ufuta kufanyika katika mfumo wa ushindani wa bei katika msimu wa mwaka 2018/2019.

Mfumo huu umeleta tija sana kwa wakulima kwa kuongezeka kwa bei ya soko ukilinganisha na msimu uliopita ambapo ufuta ulinunuliwa kiholela bila kuwa na usimamizi na mkulima kupata bei ndogo ambayo haikuzidi shilingi 2500 kwa kilo ukilinganisha na msimu huu ambao bei yake ni zaidi ya shilingi 3000 kwa kilo.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Tunduru Diwani wa Kata ya Marumba ambapo mnada wa pili ulifanyika katika Amcos ya Mtiti  Mh.Msenga S.Msenga aliishukuru serikali kwa wakulima wa ufuta kulipwa kwa wakati fedha za zao la ufuta kwa kupata bei nzuri.

"tunaishukuru serikali kufanya usimamizi wa zao la ufuta, hapo awali zao hili liliuzwa kiholela sana na kwa bei ndogo hatukuwahi kuuza kwa bei kama za mwaka huu,mkulima anapata hadi shilingi 3000 kwa kilo,lakini pia wakulima wanalipwa kwa wakati kwani ndani ya wiki moja tuu baada ya mnada" alisema Diwani wa Marumba Msenga S.Msenga.

Afisa Ushirika wilaya George Bisani pamoja na ndg Imani Kalembo wakifungua sanduku la zabuni katika mnada wa pili wa Ufuta uliofanyika Marumba

Akizungumza na wananchi wakati wa mnada wa pili Katibu Tawala wilaya ya Tunduru Ndg Ghaibu Lingo alisema jumla ya kilo 478,393 ziliuzwa kwa bei ya shilingi 3066.17 ambapo jumla ufuta wenye thamani ya  shilingi 1,466,833,829.00 uliuzwa kwa kampuni ya Alphakrust ltd.

Katibu Tawala alisema katika mnada wa kwanza wa ufunguzi wa uuzwaji wa zao la ufuta wilayani Tunduru  uliofanyika katika Kata ya Lukumbule jumla ya kilo 239,368 ziliuzwa kwa bei ya shilingi 3080 ambapo jumla ya ufuta wenye thamani ya shilingi 737,253,440.00 ziliuzwa kwa kampuni ya Sunshine ltd.

Alitoa tahadhari kwa wakulima ambao wanafanya udanganifu kwa kuweka mchanga kwenye ufuta ili kuongeza uzito, serikali haitosita kumchukulia hatua kali za kisheria ili kukomesha tabia hiyo.

Hata hivyo Mnada wa pili wa ufuta wilaya ya Tunduru ulifanyika katika Amcos ya Mtiti iliyopo kata ya Marumba wilayani Tunduru ambapo wanunuzi wapatao 8 walijitokeza kwa ajili ya kununua ufuta wa wakulima.

Mwisho.


Theresia Mallya

Imetolewa na Afisa Habari

Halmashauri ya Tunduru.


Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.