• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Wakulima wa Korosho Walalamikia Malipo.

Imewekwa : February 19th, 2018

Kufuatia usumbufu kwa wakulima wengi wa zao la Korosho juu ya malipo yao, wamekuwa na malalamiko mengi sana ambayo yamekuwa yakiwakilishwa katika Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kupitia Idara ya Kilimo na Ushirika  kwa kushirikiana na chama kikuu cha ushirika  Tunduru (TAMCU).

Wakulima wengi wamekuwa wakilalamika kutokulipwa na wengine malipo yao kucheleweshwa kutokana na sababau mbalimbali ikiwemo ya muongozo wa serikali wa kutaka kila mkulima kufungua Akaunti benki ndipo aweze kulipwa.

Aidha ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Tunduru amekuwa akitatua changamoto hizo kila wakati na kuwaisadia wakulima kupitia idara ya kilimo na ushirika kupata msaada awa njia bora za kuweza kupata malipo yao ikiwa ni pamoja na kufungua akaunti benki kwa kila mkulima ili haki iweze kutendeka.

Mkulima Ndg Saidi kutoka Kata ya Mchuluka anayedai kutokulipwa malipo yake ya mnada mmoja hali ambayo sio kweli baada ya uchunguzi kufanyika katika taarifa za chama cha Msingi Nakatete.

Akiendelea kutoa changamoto za wakulima mbalimbali wanazowasilisha afisa ushirika wilaya Ndg Peter Malekela amesema kuwa wakulima wengi wamekuwa na madai ambayo kwa uhalisia yanakuwa haya ukweli ndani kutokana na uelewa mdogo wa matumizi ya malipo ya kutumia benki.

Akitolea mfano wa mkulima Ndg Saidi kutoka Kata ya Mchuluka ambaye anadai kutolipwa fedha zake kwa baadhi ya Minada wakati ameshalipwa fedha zake zote baada ya uhakiki uliofanywa na Ofisi ya Ushirika kupitia chama cha Msingi Nakatete.

Afisa Ushirika wilaya alikemea kwa vikali sana tabia ya baadhi ya wakulima kutoa taarifa za uongo kwa uongozi wa wilaya ya kutokulipwa fedha zao ilihali wameshalipwa kwani endapo itabainika mkulima anaidanganya serikali ili kulipwa mara mbili atachukuliwa hatua za kisheria.

Hii ni stakabadhi ambayo aliiwakilisha Mkulima kutoka kata ya Mchuluka Amcos ya Nakatete aliyoiwasilisha katika Ofisi za Ushirika wilaya kudai malipo ambayo tayari alishalipwa.

 Na kwa upande wa mwenyekiti wa chama cha msingi Amcos ya Nakatete Ndg Kimaro alisema kuwa anakumbana na idadi kubwa ya wakulima kudai malipo mara mbili mbili na baadhi ya wakulima wenye kiwango kidogo cha mazao chini ya kilogram hamsini wanakuwa wasumbufu sana.

alisema Kimaro "wakulima hawa wamekuwa wasumbufu sana kiasi kwamba hata kufungua akaunti hawataki lakini wanataka malipo yao na ndio kwa asilimia kubwa hawajalipwa fedha zao na wengine kupitisha fedha kwenye akaunti za watu wengine hali inayoleta utata mkubwa"

Akizungumzia suala la mfumo wa malipo Ndg Kimaro alisema kuwa anaishauri serikali kupitia bodi ya zao la korosho kuona namna nzuri ya kuwalipa wakulima wanaokuwa na uzalishaji mdogo na kutoa elimu zaidi ili wakulima wengi waweze kufungua akaunti.

pia aliendelea kusema kuwa wakulima wengi wamekua na tabia ya kutoa fedhazao zote wanapokuwa wanalipwa hivyo baada ya kuzitumia na kwisha wanaanza tena wanajisahau na kuona kana kwamba hawajalipwa fedha zao hivyo kuleta usumbufu mkubwa kwenye vyama vya msingi na Halmashauri kwa ujumla.

"madai mengine wanayodai wakulima yana uhalili kwa sababu kuna ambao bado hawajalipwa mpaka sasa ambao majina yao yametoka na yamebandikwa katika mbao za matangazo katika vyama vyo vya msingi kwa ajili ya kulipwa fedha zao tayari" alisema Ndg Kimaro

wakulima mnaombwa kuzingatia sheria, kanuni na Taratibu ili kuweza kupata haki zao ikiwa ni pamoja na kulipwa fedha za korosho, hivyo miongozo inayotolewa na serikali ni vyema ikazingatiwa ili kuiendeleza wilaya Tunduru.



Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.