• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WAKULIMA mbaazi Tunduru waingiza zaidi ya bilioni 10

Imewekwa : September 29th, 2023

Wakulima wa Mbaazi wilaya ya Tunduru  wameingiza zaidi ya bilioni 10 katika mauzo ya zao la Mbaazi kwa njia ya Stakabadhi ghalani, baada ya kufanyika kwa minada mitano ya zao hilo kwa msimu wa 2023/2024.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Meneja mkuu wa Chama kikuu cha ushirika Tunduru Ndg .Imani Kalembo  Septemba 29, 2023, amesema kwa msimu huu wa mauzo ya zao la Mbaazi  Chama Kikuu kimefanikiwa kufanya minada mitano, ambapo  tani zisizopungua 5,000 zimeuzwa katika minada hiyo, na kufanya zaidi ya shilingi bilioni 10 kuingia katika mzunguko wilayani Tunduru.

“kumekuwa na ongezeko kubwa la bei kwa msimu huu wa mbaazi  ukilinganisha na msimu uliopita 2022/2023” Alisema   “Ambapo bei ya wastani ilikua shilingi 868 ukilinganisha na msimu huu ikiwa shilingi 1,998”

Aidha, Meneja  Kalembo amepongeza na kushuru jitihada zinazo endelea kuoneshwa na Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt, Samia Suluhu Hassan Pamoja na Waziri wa kilimo Mhe.Hussein  Bashe,  katika kuhakikisha kuwa wakulima wananufaika na mfumo huu wa Stakabadhi ghalani kwa kuondoa wanunuzi wa kati wa mazao hayo machanganyiko ,pia amemshukuru kwa dhati Mkuu wa wilaya ya Tunduru Mhe.Wakili, Julius S. Mtatiro kwa kujitoa kwake kuwatetea wakulima wa mazao hayo ya Ufuta,Mbaazi na Korosho.

Meneja Kalembo  amesema matarajio ya Chama Kikuu  cha Ushirika Tunduru ni kukusanya zaidi ya tani 8,000 kwa msimu ujao wa zao la mbaazi, kutokana na mikakati iliyowekwa na kuahidi kuzalisha mazao yaliyo bora  ya Stakabadhi ghalani ikiwemo Ufuta, Mbaazi  na Korosho.

Msimu huu wa 2023/2024 kwa upande wa zao la Ufuta,  Chama Kikuu cha Ushirika Tunduru kilikusanya zaidi ya tani 4000, ikiwa ni zaidi ya ukusanyaji wa zao la Ufuta kwa msimu wa 2022/2023, ambapo kwa msimu wa 2023/2024 zao hilo limewaingizia wakulima zaidi ya shilingi  bilioni 17.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda, Kaimu Mkuu Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.