• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

wakandarasi wasio kuwa na uwezo, kutokuwepo kazi

Imewekwa : October 25th, 2018

Hayo yamesemwa na waziri wa Maji  Makame Mbarawa akiwa katika ziara ya siku mbili wilayani Tunduru iliyoanza tarehe 20 hadi 21 octoba 2018, na kukagua miradi mitano ya maji  inayoendelea kutekelezwa na ile iliyokamilika ya Mtina, Mbesa, Mradi wa Maji Tunduru Mjini, Nandembo na Matemanga.

Akisoma taarifa ya hali ya upatikanaji wa maji wilaya ya Tunduru mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homera alisema kuwa Halmashauri ya Tunduru ina jumla ya vijiji 157 lakini mpaka sasa vijiji vilivyofikiwa na mfumo wa huduma wa maji safi na salama ni 115 huku vijiji 38 vikiwa bado, pia ikiwa ni asilimia 64.4 ya wakazi waishio vijijini.

wananchi wa Kata ya Mtina wakimsikiliza Waziri wa Maji Mh. Makame Mbarawa  ambaye hayupo katika picha akiwa kwenye ziara ya siku mbili  ya ukaguzi wa miradi ya maji inayotekelezwa wilayani humo.

Aliendelea kusema kuwa wilaya kupitia program ya maendeleo ya sekta ya maji (WSDP)  kuanzia mwaka 2012/2013 ilianza kutekeleza miradi katika vijiji 11 ambapo miradi minne 4 imekamilika, mitatu ipo katika hatua mbalimbali za ukamilishaji na vijiji 4 maji hayakupatikana katika usanifu.

“miradi iliyokamilika inatoa huduma kwa jumla ya vijiji 12 vinanufaika na huduma ya maji safi na salama, vijiji hivyo ni Nandembo, Amka, Nangunguru, Lipepo, Chilundundu, Lukumbule,Mchesi, Amani, Meamtwaro, Mchengamoto na Chiungo” alisema Mkuu wa wilaya.

Kwa upande wa Waziri wa Maji Makame Mbarawa akiwa katika Ukaguzi wa miradi, alisema katika utekelezaji wa Ilani ya chama cha mapinduzi ya mwaka 2015/2020 serikali imedhamiria kutoa huduma ya maji safi na salama kwa asilimia 95 kwenye miji ya mikoa, 90 miji ya wilaya na asilimia 85 katika vijiji ambapo alisema kwa sasa wilaya ya Tunduru imepiga hatua kutoka asilimia 53 na kufikia 66 mjini.

Mhandisi wa maji wilaya Ndg Bartolomeo Matwiga akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi wa Maji Mbesa kwa Waziri wa Maji Makame Mbarawa.

Waziri  Mbarawa alibaini changamoto kubwa katika miradi ya maji wilayani Tunduru ni vyanzo vya  maji kukosa maji ya  kutosha baada ya miradi kuanza kufanya kazi hali wakati wa usanifu vilionekana kuwa na maji, “hali hii inaweza kuchangiwa na uharibifu wa mazingira unaofanywa na wananchi kwa kukata miti, vilevile mabadiliko ya tabia ya nchi, niwaombe wananchi kutunza na kuvilinda vyanzo vya maji ili miradi hii iwe endelevu”

Aidha aliwataka wakandarasi wote wanaotekeleza miradi ya maji ya Mtina na Matemanga kukamilisha kwa wakati ili wananchi waweze kupata huduma ya maji na kuondoa adha ya wanawake kutembea umbali mkubwa kutafuta maji kwani ilani ya CCM inataka mwananchi asipate huduma ya maji kwa umbali usiozidi mita 400.


Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.