• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WAHUDUMU WA AFYA WAPATIWA MAFUNZO YA LISHE WILAYANI TUNDURU

Imewekwa : November 9th, 2024

AFISA LISHE ATOA ELIMU YA LISHE KWA WAHUDUMU WA AFYA WILAYANI TUNDURU.

Katika juhudi za kuboresha huduma za afya na lishe katika jamii, Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru imewapa mafunzo wahudumu wa afya kuhusu umuhimu wa lishe bora na uhusiano wake katika kuepuka udumavu na magonjwa yanayotokana na lishe duni. Mafunzo haya yameongozwa na Afisa Lishe Wilaya ya Tunduru ndg. Martini Kigosi. Aidha mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru siku ya tarehe 08/11/2024 na yalihusisha wauguzi, na wahudumu wengine wa afya.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Afisa Lishe Wilaya ya Tunduru Martini Kigosi alieleza kuwa lishe bora ni msingi muhimu katika kuzuia magonjwa mengi ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza kama vile kisukari, shinikizo la damu, na utapiamlo. Aliongeza kuwa wahudumu wa afya wanahitaji ujuzi wa kutosha kuhusu lishe ili waweze kutoa huduma bora na ushauri kwa wagonjwa wao na wananchi kiujumla hasa katika matibabu ya magonjwa yanayotokana na lishe duni.

Mafunzo yalijikita katika maeneo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na:

Jinsi ya kuwahudumia walengwa wa siku 1000 ambao ni kina Mama wajawazito, kina mama wanaonyonyesha na watoto chini ya miaka miwili kwa kuzingatia huduma bora za afya na lishe.

Jinsi ya kuwagundua watoto wenye utapiamlo mkali na matibabu ya watoto wenye utapiamlo mkali.

Jinsi ya kufanya tathmini ya hali ya lishe kwa watoto chini ya miaka mitano kwa kuwapima udumavu, ukondefu na uzito pungufu.
Ujazaji wa taarifa za afua za lishe ngazi ya kituo kwa usahihi na umuhimu wa kujaza taarifa kwa usahihi.

Bi.Leonatha Lutego, Maratibu huduma za afya ya Uzazi,Mama na Mtoto Wilayani Tunduru aliongeza kwa kusema kuwa wahudumu wa afya wanalo jukumu kubwa la kuwaelimisha wananchi kuhusu lishe bora na matumizi sahihi ya vyakula ili Kuondokana na tatizo udumavu.
Mafunzo haya yanatarajiwa kuleta mabadiliko chanya katika utoaji wa huduma za afya kwa jamii, na pia kuongeza ufanisi katika kudhibiti magonjwa ambayo yanatokana na matatizo ya lishe.

Mwisho.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.