• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

WACHIMBAJI wadogo wa madini wa wilaya ya Tunduru,wameiomba Serikali kuangalia upya sheria ya Madini

Imewekwa : July 17th, 2019





WACHIMBAJI wadogo wa madini wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma,wameiomba Serikali kuangalia upya sheria  inayotaka leseni zote za madini kufanya kazi katika eneo husika.

Wameeleza kuwa,sheria hiyo imesababisha Biashara ya Madini kudorola na baadhi ya wanunuzi wakubwa wa madini kukimbia na hivyo Serikali kukosa  kodi na ushuru.

Wakizungumza jana, katika kikao cha kujadili juu ya mwenendo wa sekta ya  madini na kero zinazo wakabili wadau wa Madini wilayani Tunduru wadau  hao  walisema, sheria hiyo inatengeneza mazingira kwa baadhi ya watu kutumia njia mbadala kutafuta soko  na hivyo kuikosesha Serikali mapato.

Mathew Ngonyani alisema, sheria ya kuzuia madini kuuzwa  katika eneo husika imesaidia sana kudhibiti udanganyifu na vitendo vya wizi,lakini haiwasaidii sana wachimbaji wadogo kwa kuwa baadhi ya madini yanayopatikana Tunduru soko lake liko nje ya Tunduru na mkoa wa Ruvuma.

Naye Mjumbe wa Chama cha wachimbaji Madini wilaya ya Tunduru Mohamed Rojas alisema,  kuna aina  50 ya Madini yanayopatikana katika wilaya hiyo, hata hivyo aina 10  tu ambazo soko lake liko Tunduru na yanayobaki soko  linapatikana  mikoa mingine kama Arusha,Dar eslaam, na Maganzo mkoani Shinyanga.

Kwa mujibu wake, kuzuia kuuza madini  hayo nje ya mkoa wa Ruvuma ni kuifanya kazi hiyo kuwa ngumu sana kwa Madalali(Mabroka) na wachimbaji wadogo ambao wanategea kazi hiyo kuendesha maisha yao ya kila siku ambapo wameiomba Serikali iangalie namna Bora ya kuruhusu Madalali na wachimbaji wadogo kwenda kuuza madini nje ya mkoa.

Rojas alisema,soko la madini lililopo Tunduru limekuwa na changamoto nyingi na kwa sasa sio rafiki tena, kwa kuwa Biashara  hiyo inahitaji siri kubwa kwa muuzaji na mununuzi, kitendo cha kutumia chumba kimoja wanunuzi zaidi ya mmoja ina changia wachimbaji kushindwa kupata Bei nzuri.

Aidha,ameiomba Halmashauri ya wilaya ya Tunduru kuharakisha upatikanaji wa jengo Bora na lenye nafasi ili wanunuzi wakubwa wapate sehemu sahihi na Bora kwa ajili ya biashara hiyo.

Akijibu malalamiko hayo Katibu Tawala wa wilaya ya Tunduru Ghaib Lingo alisema, tayari Serikali imeshapa jengo kubwa ambalo litatumika kwa ajili ya ununuzi na uuzaji wa Madini yote  yanayochimbwa katika wilaya hiyo.

Kwa mujibu wake,Serikali haijakataza wachimbaji na madalali kwenda kuuza madini nje,isipokuwa imewataka kufuata sheria ikiwemo kuwa na leseni inayoonesha kuwa uhalali wa madini hayo sambamba na vitambulisho vya wajasilimali kwa wachimbaji wadogo.

Pia, amewashukia wachimbaji wadogo na madalali hao kutokana na tabia yao ya kukwepa kulipa kodi na wengine kudiriki kuficha madini ambapo amesisitiza kuwa,serikali ya wilaya kwa kutumia kikosi kazi itahakikisha inawakamata na kuwachukulia hatua wale watakao kutwa wanauza madini nje ya vituo rasmi vilivyowekwa na Serikali.

Lingo ametoa siku kumi kwa wanunuzi wa madini,kuondoa haraka mabango ya matangazo yaliyowekwa kwenye  nyumbani zao na kando kando ya Bara bara, kwa kuwa yanatumika sana kuuza na kununulia madini kinyume na utaratibu.

Amewataka wachimbaji wadogo,kuchangamkia fursa ya kutolewa vitambulisho vya wajasilimali ili kuepuka  usumbufu kutoka kwa Mamlaka ya Mapato (TRA) na vyombo vya dola pindi vitakavyoonza operesheni ya kuwasaka  watu wanaokwepa kulipa kodi ambao mitaji yao inazidi Ml 4.

Kwa upande wake,mwakilishi kutoka ofisi ya Afisa Madini mkoa wa Ruvuma  Getty Massawe alisema, Tume ya  Madini italeta mtaalam ambaye atakuwa na kazi ya kufanya tathimini ya madeni yote na kujua thaman halisi,  kabla ya kufika kwa mnunuzi hatua ambayo itasaidia  kudhibiti udanganyifu na vitendo vya wizi wanavyofanyiwa wachimbaji wadogo.

Alisema, mchimbaji mdogo na dalali mwenye leseni  yuko huru kuuza Madini popote ndani ya Tanzania kwa kutumia masoko yaliyopo ambapo amesisitiza kuwa uuzaji wowote  wa madini  nje ya vituo vilivyowekwa na Serikali ni kosa kubwa.

Naye Afisa Migodi wa Madini kutoka Ofisi ya Madini wilaya ya Tunduru Juma Kapera alisema, ofisi ya madini kwa kushirikiana na Chama cha Wachimbaji Madini Tunduru wapo katika hatua ya mwisho kupata jengo ambalo litatumika kama kituo kikuu cha kuuza na kununua madini.
MWISHO





















Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.