• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

UZINDUZI wa wiki ya unyonyeshaji Tunduru.

Imewekwa : August 1st, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru imeungana na mataifa mengine duniani kwa kuzindua rasmi Wiki ya Unyonyeshaji Duniani. Uzinduzi huu umefanyika katika viwanja vya Baraza la Idd, ukiwa na lengo kuu la kuelimisha na kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa unyonyeshaji wa maziwa ya mama kwa afya bora ya watoto.

Mgeni rasmi katika hafla hii alikuwa Mganga Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Daktari Wilfred Rwechungula. Katika hotuba yake, Daktari Rwechungula alisisitiza umuhimu wa kuzingatia unyonyeshaji wa maziwa ya mama pekee kwa watoto wachanga kwa kipindi cha miezi sita ya kwanza tangu kuzaliwa. Alieleza kuwa katika kipindi hicho, mtoto hahitaji kupewa maji, chakula mbadala, au vinywaji vingine, Alieleza kuwa kwa kufanya hivyo, mtoto anapata virutubisho vyote muhimu, kinga dhidi ya magonjwa, na uhusiano wa karibu na mama yake.

Daktari Rwechungula aliongeza kuwa unyonyeshaji wa maziwa ya mama unasaidia kumlinda mtoto dhidi ya magonjwa mbalimbali, unachangia katika maendeleo ya ubongo wake, na pia huimarisha kifungo cha upendo kati ya mama na mtoto. Aliwahimiza kina mama kuepuka kumpatia mtoto maji, chai, au chakula kingine chochote mbadala katika kipindi hicho cha miezi sita, kwani kufanya hivyo kunaweza kudhoofisha kinga ya mtoto na kumsababishia matatizo ya kiafya. Aliongeza kuwa maziwa ya mama yana kila kitu anachohitaji mtoto kwa ukuaji wake mzuri na salama.

Wiki hii ya unyonyeshaj inatarajiwa kutumika kama jukwaa la kuongeza uelewa katika jamii kuhusu faida za unyonyeshaji, changamoto zinazowakabili akina mama wengi, na namna bora ya kuzishinda. Waliohudhuria uzinduzi huo walipata fursa ya kupata elimu na ushauri kutoka kwa wataalamu wa afya kuhusu unyonyeshaji sahihi.

Wiki ya Unyonyeshaji Duniani, inayoangazia umuhimu wa maziwa ya mama kwa afya ya watoto, inaongozwa na kauli mbiu "Thamini unyonyeshaji: Weka mazingira wezeshi kwa mama na mtoto." Kauli mbiu hii inalenga kusisitiza kwamba unyonyeshaji sio jukumu la mama pekee, bali ni jukumu la jamii nzima. Inatoa wito kwa jamii, waajiri, na taasisi mbalimbali kuunda mazingira rafiki na yanayowezesha akina mama kunyonyesha watoto wao bila vikwazo. Kwa mfano, kuwepo kwa vyumba maalum vya kunyonyesha maofisini, muda wa kutosha wa likizo ya uzazi, na kuondoa unyanyapaa unaoweza kumfanya mama ajisikie vibaya kunyonyesha hadharani. Kwa kuthamini na kuweka mazingira wezeshi, tunahakikisha watoto wanapata lishe bora na kukuza kizazi chenye afya na nguvu.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.