• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

UJENZI SOKO LA KIMATAIFA LA MADINI YA VITO WAENDELEO TUNDURU

Imewekwa : March 1st, 2024

UJENZI WA SOKO LA KIMATAIFA LA MADINI YA VITO WAENDELEA, TUNDURU

Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru inashirikiana na wadau wa maendeleo wilayani humo kukamilisha ujenzi wa soko jipya la kisasa la madini ya vito ambalo litakuwa soko kubwa zaidi Afrika Mashariki kwa madini ya vito.

Kwa mujibu wa Chiza Marando, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, ujenzi huo ulioanza mwishoni mwa Disemba 2023 unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Aprili 2024, utagharimu Shilingi 1,087,000,000 (Bilioni 1.087) na jengo litakuwa na uwezo wa kutumiwa na kampuni 155 za madini ya vito kwa wakati mmoja.

Ndg. Chiza Marando ameweka bayana kuwa zaidi ya kampuni 130 zimeshaomba nafasi ya kufanyia biashara kwenye soko hilo na kwamba eneo la soko lina uwezo wa kubeba makampuni zaidi ya 500 ikiwa makampuni yataendelea kujitokeza.

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Wakili Julius Mtatiro akiambatana na Kamati ya Usalama ya Wilaya, ametembelea ujenzi huo na kupongeza sana hatua hiyo muhimu yenye tija kwa mustakabali wa rasilimali ambazo ziko Tanzania.

DC Mtatiro ameielekeza Halmashauri ya Tunduru kukamilisha haraka ujenzi huo na kuhakikisha soko linaanza kufanya kazi kwa wakati. Mtatiro amesema soko hili la pamoja likianza litapunguza vitendo vya utoroshaji wa madini ya vito wilayani humo, ambavyo vinafanywa na baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu na kupelekea serikali kukosa mapato na kodi.

Mtatiro amesisitiza kuwa soko hili likianza serikali haitaruhusu tena masoko madogo madogo kama Tudeco na Generation yaendelee na kazi kwani utitiri wa masoko hayo na kukosa soko la pamoja kumekuwa chanzo cha utoroshaji wa madini, biashara za madini ya vito nje ya masoko, biashara za madini ya vito majumbani, kukosa ushindani wa bei ya madini ya vito, serikali kukosa kodi na mapato na mengine madhara mengine mengi.

DC Mtatiro ameelekeza kampuni za madini ambazo zinafanyia kazi zake kwenye masoko madogo madogo ya madini wilayani humo zijiandae kuhamia kwenye Soko la Pamoja la Kimataifa la Madini ya Vito na kwamba kukiuka kuhamia kwenye soko hilo ni mbinu ya kuhujumu maelekezo ya serikali na maslahi ya nchi na kwamba serikali itachukua hatua.

Akizungumza kwenye ziara hiyo, Afisa Migodi wa Wilaya ya Tunduru Ndg. Emmanuel Bushi ameeleza kuwa Soko Jipya la Pamoja la Kimataifa la Madini ya Vito ni mkombozi wa wachimbaji wadogo wadogo wa Madini ya vito wilayani humo na kwamba watapata ushindani na bei zenye tija kuliko hivyo sasa.

Afisa huyo ameishukuru sana Serikali kwa maono makubwa na kufafanua kuwa soko hilo jipya litafanya kazi ya usimamizi wa madini ya vito iwe nyepesi kwani hakutakuwa na mianya kama ilivyo sasa ambapo wilaya ina masoko madogo madogo.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.