• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

TUNDURU yaadhimisha siku ya Lishe na Afya

Imewekwa : October 30th, 2023

Siku ya lishe na afya iliadhimishwa katika Shule ya Sekondari Tunduru, Wilayani Tunduru. Shughuli hiyo ilihudhuriwa na Afisa lishe, Afisa Ustawi wa Jamii, Mwalimu Mkuu, na wanafunzi wa shule ya Sekondari Tunduru.

Maadhimisho hayo yaliongozwa na Afisa Lishe wa Wilaya ya Tunduru, Bi. Martha Kibona, ambaye alitoa hotuba yake ya kuhamasisha wanafunzi na jamii kuhusu umuhimu wa kula vyakula vyenye virutubisho muhimu kwa ajili ya ukuaji na maendeleo ya mwili na akili.

Afisa Lishe wa Wilaya ya Tunduru, Bi. Martha Kibona, alitoa Elimu kuhusu lishe bora kwa kijana aliye katika umri wa balehe. Alisema kuwa Lishe bora ni muhimu kwa ukuaji na maendeleo yao, aliwashauri walimu na walezi wa wanafunzi kuhakikisha kuwa watoto wanapata mlo kamili unaozingatia lishe bora.

"Lishe bora ni muhimu kwa Afya njema," alisema Bi. Martha. "Wakati wa ukuaji, mwili unahitaji virutubisho muhimu ili kukua na kuendeleza akili. Vyakula vyenye virutubisho muhimu ni pamoja na matunda,mboga mboga, nafaka, na protini."

Afisa Ustawi wa Jamii Bwn. Nelson Yohana aliwaelimisha wanafunzi kuhusu maswala ya ukatili wa kijinsia na jinsi ya kuzuia ukatili wa kijinsia katika jamii. Aliwataka wanafunzi kuwa waangalifu dhidi ya ukatili wa kijinsia na.Pia aliwahimiza waweze kuripoti vitendo hivi vya ukatili ili kuepuka madhara yatokanayo na matendo hayo.

Mwalimu mkuu wa shule ya Sekondari Tunduru alitoa shukrani kwa wageni waalikwa na wanafunzi walio shiriki kikamilifu kwa kujifunza kwa bidii juu ya lishe bora na afya. Aidha, aliwashauri wanafunzi kusimamia vyema tabia na afya zao.

Hafla hii ya siku ya lishe na afya ilikuwa na manufaa makubwa kwa wanafunzi, kwani walipata elimu muhimu juu ya jinsi ya kudumisha afya bora kwa njia ya lishe bora na mazoezi. Pia walitambua haja ya kuelimishwa juu ya maswala ya ukatili wa kijinsia katika jamii. Hivyo, wanafunzi walionekana kuwa wamepata hamasa ya kuanza kuboresha lishe zao na kuwa na ubunifu wa kujipanga katika mazoezi kwa ajili ya afya bora.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.