• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

TUNDURU KUYAFUNGUA DARASA LA WANAKISOMO

Imewekwa : July 31st, 2017

Mkuu wa wilaya ya Tunduru mh.Juma Zuberi Homera afanya ufunguzi darasa la kisomo katika za msingi Mbesa na Airport zilizopo kata ya Mbesa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma.
 Akitoa hotuba kwa wanakisomo hao mh Homera alisema kuwa elimu ya watu wazima itasaidia wanakisomo kupata haki zao za msingi ikiwa watakujua kusoma,kuandika na kuhesabu hivyo kuondokana na adui ujinga katika taifa la Tanzania .
Pia kwa wananchi kupata elimu hii amabyo waliikosa kwa muda mrefu itasaidia hata katika uchaguzi wa mwaka 2020 kushiriki na kumpigia kura kiongozi unayemtaka bila ya kushawishiwa na mtu yeyote kutokana na kujua kusoma na kuandika.

kutokana na senza iliyoafanywa na TASAF imegundulika kuwa  wilaya ya Tunduru ina jumla ya watu wasiojua kusoma na kuandika ni asilimia 30, hivyo kupunguza kasi ya ushiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo na kushindwa pia kujua namna ya kupata haki zao kutokana na ukosefu wa elimu.

vilevile kutokana na mila na desturi za jamii ya Tunduru takwimu zinaonesha asilimia kubwa ya wasiojua kusoma na kuandika ni wanawake hivyo jamii inatakiwa kuondoa dhana potovu iliyojengeka miongoni mwao kuwa watoto wa kiume ndio wenye fursa ya kupata Elimu na wale wa kike wakiwaacha kwa ajili ya kuolewa na kufanya kazi nyingine za nyumbani.

akitoa taarifa hiyo mbele ya mkuu wa wilaya ya Tunduru Mh. Juma Zuberi Homera afisa Elimu Takwimu na vielelezo ndg Abdul Kazembe alisema kuwa jamii ya Tunduru inakabiliwa sana na mfumo dume na wanawatenga sana watoto wakike hivyo kumuomba mkuu wa wilaya kuhamasisha wananchi kuona umuhimu wa watoto wa kike kupata Elimu kwani wana Haki sawa na watoto wa kiume.

aidha akisoma risala kwa mgeni mkuu wa shule ya msingi mbesa alisema kuwa changamoto kubwa wananyokumbana katika kuendeleza darasa la kisomo ni miundombinu ya kufundishia ikiwa ni pamoja na ukosefu wa umeme katika shule za msingi Aiport na Mbesa, ukosefu wa darasa la wanakisomo, ukosefu wa deki na Tv kwa ajili ya kufundishia kwani ufundishaji wa watu wazima nio tofauti na elimu ya awali.

Akitoa ufafanuzi wa changamoto hizo mkuu wa wilaya Mh.Juma Zuberi Homera aliipongeza halmashauri ya wilaya ya tunduru kwa kuona umuhimu wa kuanzisha darasa la wanakisomo ili kupigana vita na adui ujinga na kuwasaidia wananchi kujua kusoma, kuandika na kuhesabu, hali hii itachochea maendeleo katika wilaya yetu na kuendana na kauli sera ya serikali ya kuboresha elimu na kutoa elimu sawa kwa wote.

Mh. homera aliguswa sana na muamko wa wananchi walijitokeza kusoma hivyo kuahidi kutoa mchango wa bati 30 kwa ajili ya kuuzeka darasa la wanakisomo, kuwapelekea wanakisomo Deki na TV ili waweze kujifunza katika mazingira wezeshi na rafiki.

Aidha kwa upande wa changamoto ya Umeme mkuu wa wilaya aliugiza uongozi wa shule kushirikiana na viongozi wa kata ili kuhakikisha kuwa umeme unafungwa katika shule ya msingi Mbesa na Airport kwa haraka.

Hata hivyo wanakisomo waliishukuru srikali kwa kuanzisha darasa la wanakisomo katika kata yao ya mbesa kwani inawasaidia kuongeza maarifa na kujua namna ya kuweza kupata huduma zao kwani wengi wao walikua hawajui kusoma na kuandika kabisa, na kuwaomba uongozi wa halmashauri kuanzisha na sehemu nyingine ili wananchi wengi wanufaike na huduma kama wanayoipata.


Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.