• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC Tunduru Aeleza namna Serikali Inavyowahudumia wananchi .

Imewekwa : July 31st, 2018

Akizungumza na wananchi wa Kata ya Kalulu wilaya ya  Tunduru Mkoani Ruvuma, katika ziara ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homera alisema serikali katika awamu tofauti imetekeleza mbali mbali ya maendeleo katika kata na vijiji vya halmashauri ya Tunduru.

Mh. Homera katika taarifa yake alisema kuwa katika sekta ya maji kata ya kalulu vijiji vya mbungulaji na rahale vimechimbwa visima vya ambapo kisima cha mbungulaji kilichowekwa jiwe la msingi na waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa tanzania Kasimu Majaliwa wananchi wanapata maji lakini kisima cha kata ya kalulu serikali imeongeza fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa kazi katika eneo ambalo maji yatapatikana kwa wingi.

Pia aliendelea katika sekta ya elimu uboreshaji wa miundombinu ya Elimu  inaendelea kuboreshwa  na Kata ya Kalulu shule ya msingi kalulu iliyopo kijiji cha rahaleo serikali inaendelea na ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa, ofisi moja na matundu nane ya vyoo ambapo mradi huu umegharimu jumla ya shilingi milioni 66,600,000 zilizotolewa na mfuko wa elimu wa matokeo makubwa EP4R, lakini katika kukabiliana na uhaba wa watumishi katika sekta ya elimu halmashauri imepokea jumla ya walimu 66 ambao wanaendelea kuripoti na shule ya msingi Kalulu  ni mojawapo ya shule walizopangiwa walimu.

Naibu waziri wa Maliasili Utalii Mh. Japhet Hasunga akiongea na  askari wanyamapori Kanda ya Kalulu wakati wa ziara ya ufuatiliaji na uendelezaji wa Vivutio vya Utalii na Malikale mikoa ya kanda ya Kusini.

Juma Homera aliendelea kusema kuwa katika kuboresha ubora wa huduma za afya serikali imeendelea kuajiri watumishi wa afya, halmashauri ya tunduru impangiwa jumla ya watumishi wa afya 90 ambao watapangiwa katika zanahati na vituo vya afya na zahanati ya Rahaleo ni watapangiwa mtumishi ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi, lakini pia serikali inaendelea na upanuzi wa majengo katika kituo cha afya kilichopo makao makuu ya tarafa Matemanga ili huduma za mama na mtoto, upasuaji mdogo, na upatikanji wa mashine ya mionzi ya kupima ujauzito (Ultrasound). 

Aliendelea kusema kuwa serikali inaendelea na usambazaji wa umeme vijijini  REA III na kijiji cha rahaleo na mbungulaji vipo katika mpango huu, hivyo niwatake wananchi kutumia fursa ya kufika kwa umeme katika kata ya Kalulu kuanzisha viwanda vidogo vidogo ili kuweza kujiendeleza kiuchumi na kukuza kipato.

vilevile Mh. Homera aliwataka wananchi wa kata kata ya Kalulu kujikita katika kilimo cha zao la ufuta ili kuweza kushiriki kwa ukamilifu katika msimu ujao wa mazao mchanganyiko na kuingia katika mfumo wa stakabadhi ghalani ambapo mikoa ya Lindi na Mtwara kwa Mwaka huu walifanikiwa sana.

Hata hivyo mkuu wa wilaya ya Tunduru aliwataka wananchi wa kata ya Kalulu kutokulima mazao yanayopendwa na wanyamapori kama Ndovu na Tembo ili kuepuka mazao yao kuliwa na wanayama hao, pia wananchi kutokufanya kilimo kando kando na hifadhi.




 

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.