• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

“TOENI taarifa zinazohusu vitendo au viashiria vya rushwa na ukiukwaji wa Sheria, taratibu na kanuni za Uchaguzi”-Bwana George Njogolo, Mkuu wa TAKUKURU Tunduru

Imewekwa : August 13th, 2024

Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Wilaya ya Tunduru, Bw. George Alanus Njogolo, Azungumza na waandishi wa habari mapema leo ofisini kwake, Lengo ni kuwashirikisha waandishi wa habari mbinu mbalimbali ambazo ni muhimu katika kufikisha ujumbe ili kuwaeleimisha wananchi juu ya Mapambano dhidi ya rushwa kabla ya uchaguzi,katika kipindi chenyewe cha uchaguzi na hata baada ya kipindi cha uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Akizungumza katika kikao hicho Bwn Njogolo amesisitiza kuwa rushwa ni adui wa maendeleo na inapaswa kupigwa vita kwa nguvu zote, ametoa wito kwa waandishi wa habari kuwasisitiza  wananchi kutoa ushirikiano katika kupambana na vitendo vya rushwa. Amewataka wananchi kuripoti mara moja kwa TAKUKURU au vyombo vingine vya sheria wanapogundua vitendo vya rushwa. Amewahakikishia kuwa taarifa zao zitalindwa.

 “Tunategemea ninyi ndio mnaowafikia wananchi kwa kiwango kikubwa na kwa wakati mmoja, kwahiyo kama mtashirikiana vyema pamoja na TAKUKURU katika kufikisha Elimu tutaifikia jamii kwa kiwango kikubwa sana” Alisema Bwn Njogolo “Kila mwananchi ana wajibu na haki ya kuchagua kiongozi amtakaye kwa ajili ya maendeleo, tutoe taarifa za vitendo vya rushwa na ukiukwaji wa sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi kwa wagombea, wananchi lakini hata kwa viongozi mbalimbali ambao tunashiriki katika zoezi zima la uchaguzi kwa mwaka huu”

Aidha, amezitaja sababu mbalimbali zinazopelekea kuwepo kwa rushwa au viashiria vyake kipindi cha uchaguzi,ikiwa ni pamoja na ukosefu wa maadili kwa jamii, kutokuwepo kwa mifumo sahihi ya kudhibiti, kuwepo kwa fursa ya kukiuka kanuni bila kubainika, misukumo ya kupita bila kupingwa na pia uelewa mdogo kwa wananchi

Bwn Njogolo aliwasisitiza waandishi wa habari kutoa taarifa muhimu kwa wananchi ili wakati utakapofika waweze kujitokeza na kujiandisha kwa wingi ili kutimiza na kutumia haki yao ya kuchagua kiongozi bora, na pia wachague kiongozi ambaye hatotumia aina yoyote ya ushawishi kama fedha au vitu kuwarubuni ili wamchague, kufanya hivyo watajikuta wanachagua kiongozi ambaye hana manufaa kwa jamii husika, aliongeza kusema, kiongozi bora ni yule atakayepita kutokana na uwezo wake wa kazi ya kuhudumia wananchi kwa uadilifu.

Wananchi wanatakiwa kuwa tayari kutoa taarifa katika vyombo vya sheria, na pia wasiogope kutoa taarifa wanapohitajika kwasababu lengo ni kutaka kushirikiana ili kuweza kuzuia na kupambana na rushwa. Pia waonapo viashiria vyovyote vya rushwa kutendeka wanatakiwa kupiga simu mara moja kupitia namba 113, kupiga namba hii ni bure na sio lazima kutaja jina lako, njia nyingine ya kueleza lalamiko ni kufika ofisi ya TAKUKURU moja kwa moja, Taarifa zako zitalindwa.

Imetolewa na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru,

Orpa Kijanda.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.