• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

TEMBO TISHIO KWA MIRADI YA TASAF -TUNDURU

Imewekwa : August 14th, 2019


Hayo yamesemwa na wananchi wa kijiji cha Mpanji wakati wa kikao cha kujadili njia za kupambana na wanyama hao ambao wamevamia miradi ya mabwawa ya samaki iliyotekelezwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2017/18 na mwaka 2018/2019.

Miradi hii ya ufugaji wa samaki katika mabwawa ni miongoni mwa miradi mingi inayotekelezwa na Mpangi ikiwa na  lengo la kuongeza kipato kwa wanufaika wa kaya maskini wilayani Tunduru ili kuweza kujikwamua kiuchumi.

Akitoa taarifa ya uharibifu uliofanywa na wanyapori katika mabwawa ya kufugia samaki  Afisa Mtendaji wa kijiji cha Mpanji Bwana Joseph Juma alisema tembo wameanza kuingia katika maeneo ya mabwawa ya kufuga samaki toka tarehe 19/04/2019 mpaka sasa ambapo hufika kila baada ya siku mbili.

katika picha ni muonekano wa bwawa la kufugia samaki katika kijiji cha mpanji lililoharibiwa na tembo wanaofika katika eneo la mradi huo kwa jili ya kupata maji.

Lakini tembo hao hufika kwa makundi kuja kunywa maji katika mabwawa hayo, hali hii kwa hapo nyuma haikuwahi kutokea mpaka Februari mwaka 2019 ndio wameanza kuonekana katika maeneo mbalimbali ya kijiji ikiwemo kufika katika mabwawa hayo ya kufugia samaki.

Aidha aliendelea kusema kuwa katika kipindi cha mwezi julai 2019 tembo wamekuwa wakionekana katika eneo la mradi wa mabwawa ya kufuga samaki kila baada ya siku mbili ambapo hufika kunywa maji wakiwa katika makundi hali iliyopelekea kupasua  mabwawa ya kufugia samaki  na hakuna tumaini la uwepo wa samaki tena.

Joseph Juma alisema wanyama hawa wamekuwa ni hatarishi kwa maisha ya wananchi wa kijiji cha Mpanji kwani hata wanashindwa kufanya shughuli za maendeleo ikiwemo kilimo kutokana na tembo kuonekana katika eneo hilo mara kwa mara.

“mradi huu wa ufagaji wa samaki sio rafiki katika mazingira yetu kwani hauna tija na unatishia Amani na hatarishi kwa maisha ya jamii, tunashindwa hata kwenda kufanya kazi mashamabni kutokana na hofu ya kukutana na tembo kwani wanazagaa katika mazingira yetu”alisema mjumbe wa Halmashauri ya kijiji ndg Rashidi.

Timu ya wataalamu wa Tasaf kutoka makao makuu na wataalam kutoka ofisi ya Mkurugenzi mtendaji wilaya wakiwa katika ukaguzi na kufa nya tathimini ya uharibifu uliofanywa na Tembo katika  mradi wa ufugaji wa samaki katika kijiji cha Mpanji. 

Athari kubwa iliyojitokeza katika mradi wa ufugaji wa samaki katika mabwawa ni kupoteza samaki waliokuwa waanze kuvunwa, kupoteza Imani na mradi wa bwawa la samaki.

Kwa upande wake kaimu Afisa wanyapori wilaya Bw. Dunia Almasi alisema sababu kubwa ya tembo kufika katika kijiji na kufanya uharibifu ni kutokana na kijiji hicho kupakana na hifadhi ya misitu ya Sasawala lakini pia eneo hilo lipo ndani ya ushoroba wa  Seleou - Niasa hivyo ni njia ya wanyamapori.

Halikadhalika  hali ya hewa ya ukame katika hifadhi inachangia  Tembo kutoka katika hifadhi kutafuta maji na Tembo ana uwezo mkubwa sana wa kunusa harufu ya maji, hivyo hufika katika eneo la mabwawa kufuata maji.

Ndg Dunia aliwashauri wananchi wa kijiji cha Mpanji kutumia njia za asili ili kuwafukuza tembo mbali  katoka mazingira yao ikiwa ni pamoja na kuchanganya pilipili, jivu na oil chafu katika vitambaa na kutundika katika miti kuzunguka eneo la mradi.

Vile vile kupanda pilipili kuzunguka eneo la mradi wa mabwawa ya samaki na kuweka mizingia ya nyuki ambao watakuwa walinzi wa kufukuza tembo kufika katika eneo hilo kwani pilipili ikimuingia tembo machoni huwashwa na kubadilisha njia.

picha ya pamoja ya viongozi wa halmashauri ya kijiji cha Mpanji na wataalam kutoka Tasaf  makao makuu, ofisi ya mkurugenzi mtendaji baada ya majadiliano na kufanya tathmini ya uhabifu uliofanywa na Tembo katika mabwawa ya kufugia samaki.

Hata hivyo ni wakati wa serikali kuchukua hatua za makusudi kunusuru maisha ya wananchi wanaozunguka maeneo ya hifadhi kwani imekuwa ni changamoto kubwa na hofu kwa wananchi na mali zao kwani wanyamapori hao wanaonekana katika makazi ya wananchi mara kwa mara, vilevile taasisi zinazojishughulisha na uhifadhi wa wanayamapori kutoa aelimu kwa wananchi ya njia bora za kukabiliana na wanyama waharibifu kama hawa ili miradi inayotekelezwa iwe indelevu.

  

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.