• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

TANI 4,017 za Korosho zimeuzwa mnada wa Pili Tunduru.

Imewekwa : November 9th, 2023

Wakulima wa korosho Wilayani Tunduru wamekubali kuuza korosho zao   Tani 4,017 katika mnada wa pili wa zao hilo.

Mnada huo ulifanyika katika kijiji cha Amani  chama cha ushirika cha msingi  CHAMANA (CHAMANA AMCOS), kupitia Mfumo wa Stakabadhi ghalani, Novemba 09, 2023, chini ya Chama kikuu cha Ushirika Tunduru TAMCU LTD.

Wananunuzi 18 walionesha nia ya kununua  Korosho  Tani 4,017 ambazo ziliingia sokoni katika mnada huu wa pili, wanunuzi watano walishinda kununua Korosho hizo zilizopo ghalani kwa bei ya shilingi 1,831 kwa kilo.

Akizungumza baada ya kutangaza bei hiyo ya zao la korosho Mwenyekiti wa Chama kikuu cha Ushirika TAMCU LTD   Ndg. Mussa Manjaule amewasihi wakulima kutotegemea  zao moja la kibiashara na kuwataka kulima kilimo cha mazao mchanganyiko, na kuviomba vyama vya msingi kulipa fedha za wakulima kwa wakati.

Mwenyekiti wa Chama kikuu cha Ushirika cha Mazao Tunduru  Ndg . Mussa Manajaule, akizungumza katika mnada wa pili wa zao la Korosho.

“ Viongozi  na watendaji wa vyama vya msingi tujitahidi kulipa wakulima ndani ya siku saba ambazo zimepangwa   , kwani fedha hizo  ni muhimili muhimu kwa wakulima hawa, zinakwenda  kumsaidia mkulima katika mahitaji yake ya kila siku”

Kwa upande wake Mlajisi Msaidizi wa vyama vya Ushirika Mkoa wa Ruvuma Bi. Peja Muhoja  amewasisitizia viongozi na watendaji wa Vyama vya Ushirika vya msingi kufanya majukumu yake kwa kufuata Miongozo ,sheria na kanuni zilizoweka kwa uaminifu na uadilifu,

Naye Meneja Mkuu wa Bodi ya Korosho Wilaya ya Tunduru Bi. Shauri Mokiwa amewasisistiza wakulima kuzingatia ubora na Usafi  wa korosho wanazaopeleke ghalani, kwani ubora na usafi wa korosho  unakwenda kuongeza thamani ya Korosho zetu katika sokoni.

Zaidi ya Bilioni 11 ziliingia katika mzunguko katika Wilaya ya Tunduru kupitia mnada wa kwanza wa zao la Korosho kwa msimu huu wa 2023 -  2024, ambapo wanunuzi 35 walionesha nia ya kununua korosho hizo tani 3,500 ambazo zilinunuliwa kwa shiliingi 1,994 kwa kilo.   

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.