• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

SUA yaahidi Mifuko 100 ya Saruji kuanza ujenzi wa zahanati kijiji cha Darajambili

Imewekwa : August 19th, 2018


Hayo yamesemwa na makamu mkuu wa Chuo kikuu cha Kilimo Sokoine Prof Raphael Chibunda wakati akiongea na wananchi wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma katika hafla Fupi ya makabidhiano ya majengo ya kambi ya daraja mbili kwa ajili ya kuanzisha tawi la chuo hicho wilayani Tunduru, aliahidi kutoa mchango wa mifuko ya saruji 100 ili kuanzisha ujenzi wa Zahanati katika kijiji cha darajambili.

Prof Chibunda alisema chuo kipo tayari kutoa mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya kuanza ujenzi wa zahanati katika kijiji cha darajambili ili kutoa huduma za haraka za afya kwa wananchi na wanafunzi watakaoajiunga na chuo katika kampasi ya Tunduru kwani watakuwa wananishi katika mazingira ya kijiji hicho.

“Chuo kipo tayari kutoa mifuko 100 ya saruji mkiwa tayari toeni taarifa kwa mtumishi anayebaki hapa ili taratibu za manunuzi zifanyike, zahanati itasaidia wananchi waliopo katika kijiji lakini pia wanafunzi watakaokuwa katika tawi hili na wengine ni watu wazima wenye familia zao hivyo zahanati ni lazima kujengwa”

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Tunduru Mbwana Mkwanda Sudi na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wakisaini nyaraka za makabidhiano ya majengo ya darajambili kwa ajili ya kunzaisha chuo cha kilimo sokoine kampasi ya Tunduru.

Aliendelea kusema kuwa sifa za kuijunga na chuo kikuu cha kilimo SUA ngazi ya cheti mwanafunzi anatakiwa kuwa na ufaulu wa kuanzia alama D nne na kuendelea katika mtihani wa kidato cha nne. “nawahamasisha wanafunzi kuanzia kidato cha I hadi IV kupigana kupata D4 ili kupata nafasi ya kusoma katika chuo cha SUA tawi la Tunduru”alisema Prof.Chibunda.

Naye mkuu wa wilaya ya Tunduru Mh.Juma Homera alipongeza uongozi wa chuo kikuu cha kilimo SUA kufanya maamuzi ya kuanzisha tawi katika wilaya ya Tunduru kwani fursa kubwa sana kwa mikoa ya kusini ambayo uchumi wao mkubwa ni kilimo.

Viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Tunduru kwa pamoja na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine wakionesha hati za makabidhiano ya majengo kwa ajili ya kuanza kutoa fursa mbalimbali za kufundisha katika Tawi jipya la Tunduru.wa kwanza kutoka kulia ni kaimu mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Tunduru ndg Jonathan Albano Haule, wa pili ni Mwenyekiti wa Halmashauri MH.Mbwana Mkwanda Sudi, akifuatiwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha kilimo SUA Prof.Raphael Chibunda na Mkuu wa wilaya ya Tunduru Mh.Juma Zuberi Homera.

Mh. Homera aliendelea kusema wilaya ya Tunduru imepakana na hifadhi ya wanyamapori na pori la akiba hivyo kuanzishwa kwa tawi la chuo cha SUA kutasaidia kutoa elimu ya kutosha kwa wananchi ya namna bora ya kukabiliana na wanyama waharibifu mkoani Ruvuma.

Aidha mkuu wa wilaya aliomba kipaumbele cha kozi za kilimo kutolewa katika tawi la Tunduru ili kuendana na mahitaji ya wananchiwa Tunduru kwani kwa asilimia kubwa uchemi wao unategemea kilimo cha mazao lakini kuna upungufu mkubwa wa wataalam wa Kilimo.

Makamu Mkuu wa Chuo cha Kilimo SUA Prof.Raphael Chibunda wakishirikiana na Mkuu wa wilaya ya Tunduru Mh.Juma zuberi Homera kufungua bango la Chuo Kikuu cha Sokoine Tawi la Tunduru baada ya kusaini Mkata wa makabidhiano ya majengo.

Kwa upande wake diwani wa kata ya Namwinyu Mh.Thabiti S.Thabiti akiongea kwa niaba ya wananchi alishukuru sana kwa uamuzi uliofanywa na serikali kupeleka chuo katika kata yake , lakini pia aliahidi kutoa ushirikiano wa kila hali katika kuhakikisha kuwa wanaanza ujenzi wa zahanati mara moja.

Mh.Thabiti S.Thabiti alisema  wananchi wako tayari kutoa maeneo kwa ajili ya upanuzi wa eneo la chuo kikuu cha kilimo SUA ili kusogeza huduma ya elimu kwa wananchi wa Tunduru na wilaya jirani, alisema “hii ni fursa ambayo tumeisubiri kwa muda mrefu lakini sasa ipo kwetu kwani watu wa kusini tulisahaulika sana”

Wananchi wa kijiji cha Darajambili Kata ya Namwinyu wilayani Tunduru wakifuatilia kwa karibu maelekezzo ya mkuu wa wilaya katika hafla fupi ya makabidhiano ya Majnego kwa ajili ya kuanzishwa kwa kampasi ya tunduru ya chuo cha kilimo Sokoine.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.