• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Stadi za Maisha, Kijana Jitambue.

Imewekwa : May 29th, 2018


Na theresia mallya.

Hayo yalisemwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Tunduru Ndg Chiza Cyprian Marando wakati wa ufunguzi wa semina ya siku mbili (2) ya kutoa elimu ya mafunzo ya uelimishaji rika na stadi za maisha kwa vijana  kutoka tarafa saba za wilaya ya Tunduru yaliyofanyika katika ukumbi wa klasta Tunduru mkoani Ruvuma kuanzia tarehe 26 hadi 27.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo Kaimu Mkurugenzi alisema kuwa vijana ndio nguvu kazi ya taifa na serikali imeamua kuwekeza kwa vijana kwani ndio kundi kubwa litakaloleta mabadiliko chanya kwa jamii katika mapinduzi ya uchumi wa  viwanda.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Chiza Marando alisema  katika risala iliyosomwa na muwezeshaji ngazi ya mkoa imeeleza wazi malengo ya mafunzo haya ya ueleimishaji rika  kuwa ni  kijana kujitambua yeye ni nani, anafanya nini na ni wapi anakokwenda na kuweza kupambana na changamoto za kimaisha zinazowakumba vijana wengi waliokata tamaa.

Ndg Marando aliendelea kutanabaisha kuwa halmashauri ya wilaya ya Tunduru  katika kutekeleza sera na miongozo ya serikali imetenga fungu kwa ajili ya vijana, wanawake na walemavu ya  vijana ili kuongeza wigo wa ajira na kupunguza utegemezi, endapo vijana watafanya kazi zitakazowaingizia kipato hali ya uchumi wa kaya utabadilika na hata wa mtu mmoja mmoja.

 Alisema “umri wa kijana ni kuanzia miaka 18 hadi 35 na huu ndio muda sahihi wa kuwekeza kwani ndio unakuwa na nguvu za kukuwezesha kufanya kazi za uzalishaji, hivyo niwaombe vijana wote mliofika katika semina hii musikilize kwa makini na kuyafanyia kazi mafunzo ya ujasiriamali mtakaofundishwa na wakufunzi”

Pia aliwakumbusha nidhamu ya matumizi ya fedha na kuwa na malengo kwa kile kidogo wanachopata ili kutengeneza maisha ya baadaye, kuepuka tamaa ya vitu ambayo haviko katika bajeti yako, kwani kijana ukiwa na tabia hiyo hutaweza kufikia malengo.

Ndg Chiza Marando alisema “tumewaita hapa kuwapa elimu itakayowasaidia, vijana mnatakiwa kujifundisha, mabinti msikubali kudanganywa na wanaume ni waongo sana,angalieni ndoto zenu fanyeni kazi msisubili vya kupewa”

Sambamba na hayo alizungumzia suala la Ukimwi ambalo ni janga la taifa na limekuwa likiwatesa sana vijaa wengi kutokana na kuijiingiza katika ngono zembe wakiwa na umri mdogo, aliwaasa vijana kuwa waaminifu kwa wenza wao ili kuondokana na adha na madhila katika familia nyingi.

Aliendelea kusema kuwa unapopata maambukizi ya vizuri vya ukimwi kutokana na ngono zembe au kuchepuka unasababisha matatizo kwa mwenza wako na familia yako kwa ujumla kwani watoto ndio wanataseka kwa starehe zako na ubinafsi wako.

Alimalizia kwa kuwataka vijana kujiunga kwenye vyama vya msingi vya ushirika, “huko mnapeleka korosho zenu na makato ya shilingi 30 ya kuendesha shughuli za chama unakatwa lakini wewe sio mwanachama hivyo ukijiunga unapata nafasi ya kuweza kutoa mchango wa mawazo na pia kugombea nafasi za uongozi” alisema ndg Chiza Marando.

Nao vijana walioshiriki mafunzo hayo walisema watakayojifunza wataenda kuyafanyia kazi na kuhakikisha kuwa wanajikwamua na hali ngumu za maisha kwa kujiongozea kipata na pia kuepekana na mila potovu zilizopo katika jamii yao, hivyo elimu hii tunatarajia kwenda kuitoa kwa vijana wenzetu ili iwe endelevu.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.