• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Serikali kujenga Shule ya Wanafunzi wenye Mahitaji Maalum

Imewekwa : February 20th, 2018


Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya  Tunduru Juma Zuberi Homera alipokuwa akikabidhi baiskeli  (wheel Chair) kwa mwanafunzi mlemavu wa viungo, pamoja na mifuko kumi ya saruji ya kukarabati vyoo katika shule ya msingi Mchangani iliyopo wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma mapema leo.

Akizungumza na wananchi pamoja na vyombo vya Habari Afisa Elimu, Elimu Maalum mwalimu Albert Nakamata alitoa changamoto ya upungufu wa miundombinu kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum, na pia alisema kuwa jamii kuwaficha watoto hao hivyo kupelekea wilaya kukosa takwimu sahihi za idadi ya walemavu.

Mwalimu Albert aliendelea kusema katika shule ya msingi Mchangani kuna jumla ya wanafunzi wenye ulemavu wapatao 8 ikiwa wenye mtindio wa ubongo wanne na walemavu wa viungo wanne, kati yao saba ni wavulana na mmoja ni msichana.

Mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Zuberi Homera akikabidhi mifuko kumi ya saruji kwa ajili ya ukarabati wa vyoo katika shule ya msingi Mchangani, katika picha aliyemshika mkono mkuu wa wilaya ni Mkurugenzi wa kampuni ya DNG ltd, mkuu wa shule ya msingi Mchangani aliyefunga ushungi pamoja na Diwani wa kata ya mchanga Mh. Abdalah Hairu

Alisema mwalimu Albert "tunaomba serikali kwa kushirikiana na wadau wengine wa maendeleo tushirikiane katika kujenga shule ya wanafunzi wenye mahitaji maalum ili kuwarahisishia katika upatikanaji wa elimu na pia kutoa changamoto kwa jamii kuwapeleka watoto hao shule na kuacha kuwaficha"

Akizungumza na wananchi wa kata ya mchangani, wanafunzi na vyombo vya Habari Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Zuberi Homera Kabla ya kukabidhi kiti cha magurudumu manne (wheel chair) kwa mwanafunzi mlemavu wa viungo Shaibu Halifa Mpoto alisema kwa mwaka wa 2017/2018 halmashauri kupitia mfuko wa Elimu Tunduru imetenga shilingi milioni 7,200,000 kwa ajili ya kununua mahitaji ya wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Mkurugenzi wa Kampuni ya DNG ltd Ndg Geofrey Kalamba wanaojishughulisha na ununuzi wa Korosho akimkabidhi mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Homera Baiskeli kwa ajili ya mwanafunzi mlemavu wa viungo Shaibu Halifa Mpoto mapema leo katika shule ya Msingi Mchangani.

Juma Homera alisema fedha iliyotengwa itatumika katika kununua Wheel Chair nyingine tano kwa ajili ya wanafunzi wenye ulemavu wa viungo, mafuta, kofia na miwani ya jua kwa ajili ya wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi ili kuwaweza kuishi katika mazingira tulivu wakati wa masomo yao.

Aliendelea kwa kuipongeza kampuni ya DNG LTDs  ambao wamenunua baiskeli kwa ajili ya mwanafunzi Shaibu Halifa Mpoto, pia kuona jitihada za serikali katika kuboresha huduma za jamii na kuchangia takribani mifuko 150 ya saruji ambayo imeelekezwa katika miradi ya ujenzi katika shule, zahanati na kituo cha forodha Lukumbule.

Bi pauline Sosthenes Mdimu akiongea na wanafunzi wa shule ya msingi Mchangani kuwasisitiza umuhimu wa Elimu na kutilia mkazo katika Elimu kwani ndio ukombozi wa mwanadamu, ukishakombolewa kifikra mengine yote yanakuja.

Akitolea maelezo juu ya ukosefu wa  miundombinu ya shule kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum, mkuu wa wilaya ya Tunduru alisema serikali ina mpango mkakati wa kuanzisha ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum katika shule ya msingi Extended ili kutoa fursa ya elimu kwa kundi hili ambalo linakumbana na changamoto za kukosa haki ya kupata elimu.

"Tuna mpango wa kujenga shule ya mahitaji maalum ya wilaya ambayo itakuwa na uwezo wa kusajili wanafunzi kuanzia darasa la awali hadi sekondari, watakuwa wanakaa shuleni ili kuweza kuhudumiwa vizuri kwani kuendelea kuwaacha katika shule  Jumuishi  hawawezi kusoma kama wanafunzi wa kawaida hasa kwa kuwalenga wale wenye mtindio wa ubongo, bubu viziwi na walemavu wa akili" Juma Homera alisema

baadhi ya viongozi walioshiriki katika zoezi la kukabidhi baiskeli kwa mwanafunzi mwenye ulemavu wa viungo pamoja na Mifuko kumi ya saruji katika shule ya Msingi Mchangani.

Pia alisema mwanafunzi Shaibu Halifa Mpoto amekuwa akibebwa mgongoni na bibi yake kufika shuleni na kurudi na wakati mwingine rafiki zake ndiyo humbeba, ambaye amekuwa katika hali hiyo toka akiwa darasa la nne hadi sasa yupo darasa la saba.

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru akifanya maribio ya Baiskeli (wheel chair) baada ya kumkabidhi mwanafunzi shaibu Halifa aliyekaa katika baiskeli hiyo.

"Hali hii ndio iliwagusa wamiliki wa Kampuni ya DNG waliokuwa wananunua zao la korosho wilayani Tunduru kuona ni vyema basi wakatoa mchango wa baiskeli kwa mwanafunzi huyu ili iweze kumsaidia na kumpunuzia mzigo bibi yake aliyekuwa anambeba mgongoni kila siku kumpleka shuleni na kumrudisha nyumbani" alisema Mkuu wa Wilaya.

Naye bibi wa mtoto Shaibu Halifa Mpoto, Bi Fatu Kauma Omari alisema kuwa anaishukuru serikali pamoja na wadau wa maendeleo waliowasaidia kumpatia mjukuu wake baiskeli, pia wanafunzi kwa kutomtenga mjuu wake, pia aliwapongeza walimu wa shule ya Msingi Mchangani kwa jitihada na moyo wa upendo wanaouonesha kwa mjuu wake.




Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.