• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

RC aipongeza Halmashauri kupata hati safi

Imewekwa : July 11th, 2019

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bi Christina Mndeme ameuopongeza uongozi wa halmashauri ya wilaya Tunduru kupata hati safi katika ukaguzi uliofanywa na mkaguzi na mdhibiti mkuu wa serikali mwaka wa fedha 2017/2018 ikiwa ni matokeo ya utendaji kazi mzuri na ushirikiano wa wataalamu, madiwani na wabunge.

Akiwa  katika kikao cha baraza la madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Tunduru la kupitia taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za serikali kwa mwaka wa fedha 2017/2018  alisema mwenendo wa Halmashauri ni mzuri kwa kuangalia miaka minne  mfululizo kuanzia mwaka 2014 hadi 2018, Halmashauri ya Tunduru imekuwa ikipata  hati safi kwa kipindi cha miaka 3 mfulululizo, isipokuwa mwaka 2014/2015 ndio ilipata hata yenye mashaka.

Alisema ni vizuri Halmashauri ikaweka mpango mkakati wa kudhibiti na utunzaji wa nyaraka katika kuhakikisha kuwa wakati wa ukaguzi nyaraka zote muhimu zinakuwepo na kupewa wakaguzi.

Alisema sababu za kuwa na hoja nyingi za nyuma ambazo hazijafungwa katika Halmashauri ni ushiriki mdogo wa wakuu wa idara katika kuaandaa majibu ya hoja, kukosekana kwa ushirikiano wakati wa ukaguzi kwa wakuu wa Idara na Vitengo wakati wa ukaguzi wa hoja za serikali.

Mkuu wa mkoa huyo alikemea tabia ya baadhi wa watumishi wanaokusanya mapato kwa kutumia mashine za POS kuchelewa kupeleka fedha benki kuchukuliwa hatua haraka sababu wanahujumu Halmashauri.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Halmashauri ya Tunduru Mh.Mbwana Mkwanda Sudi alisema kuwa usimamizi utafanyika katika utunzaji wa kumbukumbu ili kuepuka hoja ambazo sio za msingi katika halmashauri

Aidha Mh. Mbwana Mkwanda Sudi alisema Halmashauri imekumbana na changamoto ya kuchangia kidogo mfuko wa wananwake, vijana na walemavu ambapo halmashauri imetoa asilimia 28 ikiwa ni kutokana na halmashauri kuwa na chanzo kimoja kikubwa cha mapato ya ndani yatokanayo na zao la korosho hivyo kukosekana na fedha hizo kumekwamisha utekelezaji wa bajeti.

Naye mkaguzi wa hesabu za serikali mkoa wa Ruvuma aliipongeza  halmsahuri kupata hati safi lakini alizitaka idara zenye hoja kuwasilisha vielelezo ili hoja zilizopo ziweze kufungwa na kutoa ushirikiano wa karibu kwa wakaguzi ili kuepuka kuzalisha hoja Zaidi.

Mwisho.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.