• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

NMB yatoa msaada Hospitali ya Wilaya Tunduru.

Imewekwa : October 5th, 2023

Benki ya NMB imetoa msaada wa vifaa katika Hospitali ya wilaya Tunduru mkoani Ruvuma ikiwa ni moja ya Lengo la Benki hiyo kurejesha faida kwa jamii na kuifikia jamii katika mahitaji yao muhimu.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi vifaa hivo Kaimu Meneja wa benki ya NMB kanda ya Kusini Ndg. Romani Degeleki amesema kama ilivyo desturi, benki ya Nmb inarudisha kwa jamii asilimia ya faida katika shughuli zinazofanywa na Benki ya NMB.

“tunafanya biashara na jamii kwahiyo kwenye faida ambayo tunaitengeneza kila mwaka tunatenga kiasi cha kuweza kurudisha kwa jamii yetu” Alisema

Vifaa ambavyo vimekabidhiwa katika Hospitali ya wilaya ya Tunduru ni Mashuka 150, Vitanda 10, Magodoro 10, Viti vyenye Magurudumu (Wheel chair) 04, Vitenga Wodi (screen cutting) 08 ambavyo kwa ujumla vina gharimu Zaidi ya shilingi milioni 10.

Akikabidhiwa vifaa hivyo mkuu wa wilaya ya Tunduru Mh.Wakili ,Julius  S.Mtatiro ameishukuru Benki ya NMB kwa kutoa msaada  huo wa vifaa katika hospitali ya wilaya kwani itakuwa ni moja ya kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya sita, pia amewataka watendaji hasa wanaokabidhiwa vifaa hivyo kutambua majukumu yao na kuweza kuvitunza vifaa hivyo.

Aidha Mhe.Mtatiro ameiomba Benki ya NMB kuendelea kuunga mkono maendeleo ya wilaya ya Tunduru kwa kuzidi kutanua msaada katika sekta nyingine muhimu kama elimu, na kuwataka kusogeza huduma zao za kifedha hasa maeneo ya vijijini.

“Kitendo mlichokifanya sio tu mmelejesha kwa jamii,bali ni shughuli ya kurejesha kwa mwenyezi mungu, Alisema “kitendo hiki ni kikubwa sana katika wilaya yetu kinaenda kuongeza tija katika sekta ya Afya”.

Kwa upande wake Kaimu mkurugenzi Mtendaji Ndg. Masanja Kengese ametoa shukrani zake za dhati kwa Benki ya NMB kwa kuunga mkono Maendeleo ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pia ametoa rai kwa taasisi zingine kuiga jitihada hizi za kusaidia jamii.

Kwa niaba ya Hospitali ya wilaya ya Tunduru Daktari Wilfred Rwechungula Mganga Mkuu (W) Tunduru ametoa shukurani zake za dhati kwa benki ya NMB kwani vifaa hivi vinaenda kusaidia moja kwa moja wananchi wa Wilaya ya Tunduru, na kuomba kuzidi kuweka kipaumbele katika huduma za Afya.

Benki ya NMB imekuwa ni miongoni mwa benki ambayo inasaidia jamii katika Nyanja za Afya, Elimu na Mazingira na kuweza kuwasogezea wananchi huduma karibu Zaidi.



Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.