• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MSIMU WA UKUSANYAJI UFUTA TUNDURU, WAFUNGULIWA RASMI

Imewekwa : May 22nd, 2024

Msimu wa Ukusanyaji wa Ufuta kwa ajili ya mauzo ya zao la ufuta katika Wilaya ya Tunduru umefunguliwa rasmi leo Mei 22, 2024.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mheshimiwa Simon K. Chacha wakati wa Mkutano wa  wadau wa zao la ufuta uliofanyika  wilayani humo.

Mkutano huo ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Madiwani, viongozi wa Vyama vya Msingi, mameneja na makarani wapimaji.

Mheshimiwa Chacha amesisitiza viongozi wa AMCOS na makarani kusimamia ukusanyaji wa ufuta kwa uadilifu ili kuleta tija kwa wakulima wa zao hilo.

“tunapokwenda kusimamia Ukusanyaji wa  zao hili , tunatakiwa kuwa na vitu vitatu, ambavyo ni  Uadilifu, Uaminifu na Ushirikiano baina yetu”. Alisema DC Chacha.

Mhe, Chacha ameongeza kuwa minada ya ufuta wilayani Tunduru itaanza Mei 30, 2024 na itafanyika kidijitali kupitia mfumo wa Soko la Bidhaa (TMX) kwa kushirikiana na Chama Kikuu cha Ushirika wa Masoko ya Mazao Tunduru (TAMCU LTD), ambapo mnada wa kwanza utafanyika katika Tarafa ya Nalasi, Kijiji cha Molandi.

Mwenyekiti wa TAMCU LTD, Ndg. Mussa A. Manjaule, amewasisitiza makarani na mameneja kushirikiana na Bodi ya Uongozi wa Vyama ili kuhakikisha usimamizi bora wa zoezi la ukusanyaji wa ufuta kwa msimu wa 2024/2025.

Meneja Mkuu wa TAMCU LTD Ndg, Marcelino Mrope amesema amehakikisha kuwa TAMCU LTD  inatoa vifaa muhimu vitavyowezesha zoezi la ukusanyaji katika maghala ya kukusanyia ufuta, vikiwemo vifungashio, mizani, vipima unyevu, usafiri, na ghala za kuhifadhia mazao.

Aidha, Mrope ameendelea kuelezea kuwa uzalishaji wa zao la ufuta umeongezeka kwa asilimia 53.09% kutoka msimu wa 2022/2023 hadi msimu wa 2023/2024, ukifikia kgs 4,800,997.20 kutoka kgs 2,548,815. Bei ya zao la ufuta pia imeimarika kwa msimu wa 2023/2024, kwa wastani wa Tshs. 3,684.54 ikilinganishwa na Tshs. 3,019.80 kwa msimu wa 2022/2023.

Msimu huu unatarajiwa kuleta manufaa makubwa kwa wakulima wa zao la ufuta wilayani Tunduru kutokana na ongezeko la uzalishaji na bei bora ya soko.


Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.