• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MPANGO WA MSITU SHIRIKISHI KWA MANUFAA YA WANANCHI

Imewekwa : May 29th, 2017

          

MPANGO WA MSITU SHIRIKISHI KWA MANUFAA YA WANANCHI.

TUNDURU

Baraza la madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Tunduru limepitisha mpango wa usimamizi shirikishi msitu pamoja na sheria ndogo za kijiji cha Ngapa, katika mkutano wa Robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2016/2917 uliofanyika katika ukumbi wa klasta uliopo wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma.

Akitoa taarifa ya mpango huo katika kikao cha baraza la madiwani Mkurugenzi Mtendaji (W) Ndg Abdallah H Mussa alisema kijiji cha Ngapa ni miongoni mwa Vijiji saba (07) vilivyoko kwenye usimamizi shirikishi wa misitu wilaya ya Tunduru.

alisema “mradi huu utavipa vijiji hivyo kumiliki misitu yao na kuingiza mapato katika vijijiji ili kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, na lengo kuu ni ukusanyaji wa mapato yatokanayo na mazao ya misitu”

aidha mradi wa usimamizi shirikishi wa misitu umefadhiliwa na shirika la WWF, na kufanya kazi pamoja na Shirika la MIPANGO, na MJUMITA katika utekelezaji wake.

Ndg Abdallah mussa aliendelea kusema kuwa katika Halmashauri ya wilaya mpaka sasa ina jumla ya vijiji sita 06 ambavyo ni Machemba, Sauti moja, Namakambale, Mindu, Songambele,na Msinji hivyo kwa kupitisha kijiji cha Ngapa basi Halmashauri itakuwa imeingia mkataba na WWF wa vijiji saba 07.

Hata hivyo aliendelea kusema kuwa mapato yatokanayo na mradi wa usimamizi shirikishi wa misitu una faida kwa vijiji kutokana na asilimia 90 ya mapato yataelekezwa katika kijiji kwa ajili ya uendelezaji wa shughuli za maendeleo ya kijiji pamoja na asilimia kumi itapelekwa katika serikali ya Halmashauri.

Naye diwani wa Kata ya Ngapa Mh Said Ally Pindu alisema wananchi watafaidika sana na msitu huo na kuongeza mapato ya kijiji husika hivyo kuchochea maendeleo ya kata kwa sababu mapato yatakayopatikana asilimia 90 yatapelekwa katika miradi ya maendeleo ya kijiji.

Hata hivyo utunzaji wa misitu na usimamizi shirikishi wa wanakijiji katika utaboresha utunzaji wa mazingira na kutunza vyanzo vya maji hivyo kupunguza uchafuzi wa mazingira na uhifadhi wa vyanzo vya maji na kuondoa  tatizo la maji kwa wananchi.

Theresia mallya.

Afisa Habari (w)


Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.