• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MOTO WATEKETEZA BWENI LA WAVULANA NANDEMBO SEKONDARI - TUNDURU

Imewekwa : October 17th, 2017


Bweni la wanafunzi wavulana katika shule ya sekondari Nandembo limeungua moto na kuteketea kwa Mali zote za wanafunzi zilizokuwamo, wakati wanafunzi wakiwa katika nyumba ya ibada.

 Akiyoa taarifa ya moto kaimu afisa Elimu Wilaya  Mwalimu Habiba mfaume alisema taarifa za kuzuka kwa moto walizipata majira ya saa moja na nusu jioni kutoka kwa uongozi Wa shule ya sekondari Nandembo za kutokea kwa moto na kuunguza bweni la wavulana.

 Ukosefu Wa kikosi cha Zima moto katika wilaya ya Tunduru umesababisha mali za wanafunzi kuteketea kwa ni walitumia tu njia za asili kama mchanga na mitungu ya gesi ya Fire extinguisher iliyopo katika maeneo ya hostel kwa kushirikiana na majirani Wa shule.

 Alisema bweni hilo walikua wanakaa wanafunzi 72 ambao vitu vyao vimeteketea kwa moto na ikiwa ni pamoja na magodoro, vitanda, madaftari na vifaa vingine vyote vilivyokuwamo ndani ya bweni hilo.

 "Bweni hili walikua wanakaa wavulana Wa kidato cha pili, NNE na kwanza ambao vifaa vyao vimeungua ni baadhi ya vitu vichache vilivyoweza kuokolewa lakini asilimia tisini vimeungua moto"

 Chanzo cha moto huo bado hakijajulikana mpaka sasa lakini tunamshukuru mungu hakuna mwanafunzi aliyeumia au kupata madhara katika ajali hiyo ya moto.

 Aidha Halmashauri ikiongozwa na kamati ya ulinzi na usalama Wilaya, mwenyekiti Wa Halmashauri na wakuu Wa idara walifika katika shule ya sekondari kukutana na uongozi Wa shule Nandembo kutoa pole lakini pia kuona njia za haraka watakazotumia kutatua tatizo hili.

 Hatua za awali zilizochukuliwa na serikali ni kuonana na uongozi mzima Wa shule na kuandaa mikakati ya kuwafariji wanafunzi na walimu waliokumbwa na janga la moto lakini pia kuandaa njia za kuwasaidia wanafunzi wale Wa kidato cha NNE ambao wanatarijia kuanza mitihani yao mwisho Wa mwezi Octoba.

 Kutafuta sehemu ya muda ambako wavulana ambao bweni lao vimeungua watakua wanakaa kwa muda wakati serikali ikijiandaa kuona namna watakavyojenga bweni jingine kwa ajili ya wavulana.

 Walimu na wanafunzi Wa madarasa mengine walitakiwa kuwasaidia wenzao waliounguliwa na madaftari yao kutoa kopi ili waweze kujiandaa na mitihani iliyopo mbele yao.

 " ni vizuri katika kipindi hiki walimu kuwasaidia wanafunzi Wa kidato cha NNE waliounguliwa na madaftari kuwasaidia kutoa kopi ya madaftari katika shule jirani za Tunduru sekondari, Mataka na Frenkweston ambao wana machine za kupiga kopi" alisema Mwalimu Habiba.

 Aidha alimalizia kwa kusema kuwa serikali itafanya tathimini ya madhara yaliyojitokeza na muandisi majenzi pamoja na Fundi umeme wameagizwa, na uongozi Wa wilaya utafika katika shule ya sekondari Nandembo Siku ya ijumaa baada ya Tathimini kufanyika.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.