• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MNADA WA KWANZA WA UFUTA, TUNDURU

Imewekwa : June 4th, 2024

Chama Kikuu cha Ushirika wa Masoko ya Mazao Tunduru (TAMCU LTD) kimefanya uzinduzi wa Mnada wa kwanza wa Ufuta uliofanyika Kijiji cha Molandi, Kata ya Marumba, Wilaya ya Tunduru Juni 04, 2024.

Mnada huo ulifanyika chini ya uongozi wa Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mhe. Simon K. Chacha, na ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Wilaya.

Mnada huu umetumia  Mfumo wa Soko la Bidhaa (TMX) kuendesha mnada kwa njia ya kidijitali. Mfumo huu mpya uliwezesha wanunuzi wanne kununua Ufuta wote Tani 701 zilizokuwa sokoni kwa uwazi na ufanisi.

Wakulima walifurahia sana kupata bei nzuri kwa mazao yao, kwani bei ya juu ilifikia 3,783 kwa kilo, bei ya chini 3,705 kwa kilo, na bei wastani 3,744 kwa kilo. Jambo la kufurahisha zaidi ni kwamba wakulima wote walifanikiwa kuuza mazao yao yote katika mnada huo.

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru aliwapongeza wakulima kwa mafanikio yao na kuwasisitiza kuendelea kuzingatia ubora na usafi wa zao la Ufuta ili liweze kushindana vyema katika soko la kimataifa. Aliwahimiza pia wazazi kutumia fedha wanazopata kutokana na mauzo ya mazao yao kuwekeza katika elimu ya watoto wao.

Mwenyekiti wa TAMCU LTD, Ndg. Mussa A. Manjaule, aliwahimiza wakulima wa Wilaya ya Tunduru kulima mazao mchanganyiko ili kuongeza tija na kipato chao. Aliamini kuwa mbinu hii itaboresha maisha ya wakulima na kukuza uchumi wa Wilaya ya Tunduru kwa ujumla.

Meneja Mkuu wa TAMCU LTD, Ndg, Marcelino Mrope, Ametoa pongezi kwa Wakulima wa Ufuta kwa kukubali kuuza ufuta wao, aidha, amewataka wakulima  kuhakikisha akaunti zao za benki, ili kupelekea ufanisi katika ulipaji wa fedha zao.

Mnada wa Kwanza wa Ufuta umeonekana kuwa na mafanikio makubwa kwa TAMCU LTD, wakulima, na Wilaya ya Tunduru kwa ujumla. Mfumo mpya wa kidijitali umeonyesha uwezo wake wa kuboresha ufanisi wa minada, na wakulima wamepata faida nzuri kutokana na mauzo ya mazao yao.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.