• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

“MIKOPO hii ikawakwamue kiuchumi: rejesheni kwa wakati ili na wengine waweze kukopa”- DC Masanja.

Imewekwa : August 11th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mheshimiwa Denis Masanja, amekabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 574,257,500 kwa vikundi 227 Hafla ya makabidhiano ilifanyika leo, Agosti 11, 2025, katika ukumbi wa Skyway, ambapo Mheshimiwa Masanja alikabidhi mfano wa hundi kwa vikundi mbalimbali vilivyonufaika.

Mikopo hiyo imelenga makundi yenye mahitaji maalum ya kiuchumi. Kwa ujumla, vikundi 50 vya wajasiriamali wadogo vimenufaika na fedha hizi. Vikundi hivyo vimegawanyika katika makundi makuu matatu: vikundi 24 vya wanawake, vikundi 21 vya vijana, na vikundi 5 vya watu wenye ulemavu. Jumla ya wanufaika ni 227.

Fedha hizi zimekusudiwa kusaidia wanufaika kuanzisha au kupanua miradi yao ya biashara. Lengo kuu la serikali ya wilaya ni kuwajengea uwezo wananchi wake kiuchumi, kuwahamasisha kushiriki katika shughuli za uzalishaji mali, na hatimaye kuinua maisha yao. Mkuu wa Wilaya aliwakumbusha wanufaika umuhimu wa kutumia mikopo hiyo kwa malengo yaliyopangwa ili iweze kuleta mabadiliko ya kweli katika jamii yao, na pia kurejesha kwa wakati mikopo hiyo.

Aidha, Mikopo hii ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru kupitia fedha za mapato ya ndani inaendelea kutolewa kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, na sasa ni dirisha la III, ambapo wananchi wameendelea kuonesha uelewa mkubwa wa kanuni mpya iliyoboreshwa ya utengaji, utoaji na usimamizi wa mikopo 10% ya mwaka 2024, vikundi vyote vilivyokopeshwa katika kanuni hii mpya vimekuwa vikifanya marejesho vizuri kulinagana na makubaliano/mikataba iliyowekwa baina ya halmashauri na kikundi.

Pamoja na changamoto ya ushiriki mdogo wa wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu kwenye mikutano ya hadhara, wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya wamejitahidi kutoa elimu na semina mbalimbali. Mafunzo hayo yamewapa wanavikundi ujuzi muhimu kuhusu utunzaji wa fedha, uwekaji wa kumbukumbu za biashara, na uwekaji wa akiba.

Kutokana na mikopo hii na mafunzo yanayoambatana nayo, wananchi wa Tunduru wameendelea kukuza biashara zao na kufikia malengo yao ya kiuchumi. Hili ni jambo la kujivunia na linaonyesha ufanisi wa mikopo hii kama chachu ya maendeleo endelevu katika wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.