• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MICHEZO KWA USTAWI WA ELIMU NA AFYA

Imewekwa : June 8th, 2017

  

WEKEZA KATIKA MICHEZO KWA USTAWI WA ELIMU NA VIWANDA TANZANIA ni kauli mbiu ya michezo ya UMISETA NA UMITASHUMTA  mwaka 2017, mashindano haya yanafanyika katika ngazi za wilaya, mkoa na kitaifa na kwa wilaya ya Tunduru mashindano haya yalianza katika ngazi ya Kata, Tarafa ili kupata wawilikilshi watakaoiwakilisha wilaya katika mkoa na baadaye taifa.

 Akizungumza na washiriki katika ngazi ya wilaya mwakilishi wa mkurugenzi mtendaji ndg George Mbisigwe Afisa Elimu Msingi Takwimu na Vifaa alisema kuwa maandalizi yamefanyika ya kutosha na wanafunzi wako tayari kwenda kushindana ngazi ya mkoa.

 Aliendelea kusema kuwa wanafunzi watashiriki katika michezo mbali mbali ikiwa ni pamoja na mpira wa pete, mpira wa miguu,mpira wa wavu, na riadha.

 Aidha ununuzi wa vifaa vya michezo vyote vimenunuliwa na maandalizi yote yamekailika hivyo anawataka washiriki kwenda kushindana na kuhakikisha wanarudi na ushindi katika michezo yote.

 washiriki wamejiandaa vizuri kwani walianza kambi kuanzia tarehe 03 hadi terehe 06 june 2017 katika shule ya sekondari tunduru, ambapo waliitimsha jana na kupatikana washiriki wa ngazi ya mkoa.

 Hata hivyo Halmashauri ya wilaya ya Tunduru inatarajia kuwapeleka washiriki katika ngazi ya mkoa watao 56, wakiongozwa na walimu 5, daktari na viongozi wa timu 3 ndio wataanza safari tarehe 07/06/2017 kuelekea Songea ambako yatafanyika mashindano kimkoa.

  "tunatarajia kkwenda kuungana na timu nyingine za mkoa wa Ruvuma ambapo kila halmashauri ya wilaya itakuwa na wawakilishi hivyo lengo letu ni ushindi na tunaenda kushindana" alisema afisa elimu takwimu na vifaa wilaya.

 Ndg Mbesigwe alisema kuwa mashindano katika ngazi ya mkoa yatafanyika kuanzia 07 june na kumalika 10 june  2017 na mchujo utafanyika ili kupata wachezaji watakaoshiriki mashindano katika ngazi ya kitaifa yakayofanyika Mkoani Mwanza kuuwakilisha mkoa wa Ruvuma.


timu ya wanafunzi na walimu wao wakiwa katika picha ya pamoja mapema wiki hii wakati wa maandalizi ya kujiandaa kwenda kushiriki michezo ya UMITASHUMTA ngazi ya mkoa, ambapo jumla ya washiriki 56 wataiwaikilisha Halmashauri ya wilaya ya Tunduru katika mashindano yatakayodumu kuanzia tarehe 07 june hadi 10 june 2016 ngazi ya mkoa mkoa kupata mchujo wa wachezaji wataowakilisha mkoa wa Ruvuma kitaifa mkoani mwanza.

timu ya wanafunzi wa shule za msingi wilayani tunduru watakaoshiriki katika michezo mbali mbali ya mashindano ya UMITASHUMTA ngazi ya mkoa, timu ina jumla ya wachezaji 56 watakaocheza michezo ya Mpira wa Miguu, Mpira wa pete, mruko ambapo kuna mruko wa juu na wa chini, pia riadha ambapo kutakua na mbio fupi na ndefu, mbio zitakua kuanzia mita 100 hadi mita 1500, mitupo ya mkuki,tufe na visahani. wanatarajia kushindana na wachezaji kutoka halmashauri zote nane za mkoa wa Ruvuma kuanzia terehe 07 hadi 10 june 2017.


Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.