• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

MATUKIO YA MBALIMBALI

Imewekwa : May 8th, 2017

MEI MOSI YALETA FARAJA KWA WAFANYAKAZI

Wafanyakazi wilayani Tunduru wameungana na wafanyakazi Tanzania na duniani kote katika kuadhimisha sikukuu ya wafanyakazi ambayo hufanyika kila mwaka mei mosi,siku ya wafanyakazi wilaya ya Tunduru ilianza kwa maandamano kutoka idara ya ujenzi hadi uwanja wa mpira wa miguu Wilaya, na kufuatiwa na ushereheshaji ulioambatana na vikundi vya Sanaa za maonesho na michezo mbalimbali.

Akisoma risala kwa mgeni rasmi Mh Juma Zuberi  Homera wakati wa maadhimisho ya kiwilaya mratibu wa sherehe za Mei Mosi ambaye pia ni katibu wa chama cha wafanyakazi Wilaya  Ndg Kassimu Dean alisema wafanyakazi wanakabiliwa na changamoto nyingi sana ikiwa ni pamoja na makato makubwa ya kodi, mishahara midogo isiyokidhi hali halisi ya maisha kwa sasa, malimbikizo ya mshahara na kutotambulika kwa waendesha pikipiki kama kazi rasmi.

Akitoa hotuba wakati wa maadhimisho ya sikukuu ya wafanyakazi Wilaya iliyanyika katika viwanja vya mpira mgeni rasmi ambaye pia ni mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mh Juma Zuberi  Homera aliwapongeza wafanyakazi wote kwa utumishi uliotukuka na uwajibikaji hasa katika kutekeleza maagizo mbali mbali ya serikali kwa wakati katika kuwahudumia wananchi na hasa katika kutatua kero za wananchi kutekeleza dhana ya utawala bora.

Mh. Homera aliendelea kusema kuwa Madai,Haki na Stahiki mbali mbali za watumishi amezichukua na anauagiza uongozi wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi nchini kuwasilisha malalamiko hayo kwa Raisi wa Jamuhuru ya muungano wa Tanzania Mh.Jonh Joseph Pombe Magufuli kwa majadiliano ili kutafutiwa ufumbuzi.

Serikali itaendelea kulipa madeni mbali mbali ya watumishi kadiri ya makusanyo yake kutokana na zoezi la uhakiki na kuwaondoa wafanyakazi hewa serikalini limekamilika.

“baada ya zoezi la uhakiki kuisha kinachofuata ni raisi kuongeza viwango vya mshahara kwa watumishi, haki na stahiki zote zitalipwa kulingano na mapato ya nchi”alisema mh Homera.

Aidha alisema kuwa usafiri wa pikipiki unatambuliwa kisheria lakini anasikitishwa sana na baadhi yao kutimiwa na majangili  katika kusafisha meno na pembe za ndovu, wengine wananshikiana na majambazi katika kutekeleza uhalifu.

Mh Homera aliendelea kusema kuwa serikali haitawafumbia macho wananchi wanaotumia usafiri huo kuvunja sharia za nchi na sharia za usalama barabarani ikiwa ni pamoja na maderava pikipiki wanaobeba mishikaki ambayo kisheria ni marufuku.

  “kwa muendesha pikipiki (bodaboda) wanaotumia usafiri huu vibaya waache mara moja kwani sharia itachukua nafasi yake endapo utakamatwa, baadhi yenu mnashirikiana na majambazi kwa kutumia pikipiki zenu pia” alisema mkuu wa wilaya ya Tunduru.

Hata hivyo alimalizia kwa kutoa zawadi za vyeti na Hundi kwa wafanyakazi hodari kwa mwaka 2017 waliofanya vizuri katika katika utendaji wa kazi katika kada mbalimbali kutoka katika idara na sekita mbali mbali za umma na binafsi Wilayani Tunduru.

 

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.