• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Maboresho ya mikopo watumishi wa Umma –Meneja NMB Tunduru

Imewekwa : August 21st, 2018

Hayo yameshwa na meneja wa benki ya NMB tawi la Tunduru Ndg Goodluck Shirima alipokuwa akizungumza na wakuu wa Idara na Vitengo alipotembelea ofisi za Halmashauri ya wilaya ya Tunduru kwa ajili ya kutoa taarifa ya marekebisho ya mikopo kwa watumishi wa umma.

Ndg shirima alisema hapo awali kabla ya maboresho mkopo kwa watumishi wa Umma ulikua na Riba ya asilimia 19 ya mkopo lakini baada ya maboresho yaliyofanyika riba sasa  itakuwa ni asilimia 17 ya mkopo kwa watumishi waliopo katika mamlaka za serikali za mitaa (LGAs).

Meneja wa NMB tawi Tunduru Ndg Goodluck Shirima (wa kwanaza kushoto)akiwa katika kikao na wakuu wa idara na vitengo wa halmashauri ya wilaya ya Tunduru mapema wiki cha kutoa taarifa ya maboresho ya mikopo kwa watumishi wa umma.

Aliendelea kusema maboresho mengine yaliyofanyika ni pamoja na kuanzishwa kwa bima kwa mkopaji ambayo itakuwa ni asilimia 0.75 ya mkopo, hii itasaidia benki kuweza kurejesha deni endapo mkopaji atapata ulemavu wa kudumu utakaosababisha ashindwe kuendelea na majukumu yake au kifo.

Ndg Goodluck Shirima alisema kuwa kiwango kabisa cha mtumishi wa umma kukopa ni shilingi laki na kiwango cha juu kabisa kwa mtumishi ni shilingi milioni 50 kulingana na kiwango chake mshahara na umri alionao kazini.

Ndg Shirima alisema  sifa za mtumishi kupata mkopo kutoka benki ya NMB ni pamoja na  viambatanisho vifuatavyo  barua ya ajira, hati ya malipo ya mshahara (current salary slip), kopi ya kitambulisho cha kazi, barua ya uthibitisho kazini, barua ya utambulisho na picha za pasipoti za kivuli cha rangi ya bluu.

Aidha alisema benki ya NMB huduma ya mikopo ya nyumba kwa watumishi ambapo mtumishi anaweza kukopa hadi milioni 700 kulingana na kipato chake na kujenga nyumba ya ndoto yake kwa kipindi cha muda mfupi.

Akizungumza kuhusu marejesho ya mkopo wa NMB ndg Shirima alisema kuwa mkopo wa nyumba wa NMB unaweza kurejesha kwa kipindi cha hadi miezi 71 ukilinganisha na ilivyokuwa awali kabla ya maboresho, pia mtumishi unaweza kuchukua mkopo na kufanya ujenzi sehemu yeyote ndani ya ardhi ya Tanzania.

wakuu wa idara na vitengo wakiwa katika kikao na uongozi wa NMB tawi la Tunduru

Kwa upande wa Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Tunduru Ndg Jonathani Albano Haule aliwashukuru Benki ya NMB tawi la Tunduru kufika kutoa taarifa za maboresho lakini watumishi watatumia fursa iliyotolewa na benki katika kufikia malengo yao.

Kaimu Mkurugenzi alimalizia kwa kusema kuwa wana uhakika elimu iliyotolewa kwa wakuu wa idara na vitengo itawafikia watumishi walio wengi wenye sifa za kukopa, kupitia wakuu wao taarifa zitakuwa zimewafikia watumishi wote.

Theresia Mallya.

Afisa Habari Tunduru DC.

0764287387

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.