• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Maafisa tarafa Lukumbule na Nampungu simamieni utatuzi wa mgogoro wa mipaka Machemba - Azimio.

Imewekwa : May 15th, 2019

Na Theresia Mallya- Tunduru

15/05/2019

Akiwa katika mkutano wa hadhara kijiji cha Azimio mkuu wa wilaya ya Tunduru Mhe.Juma Zuberi Homera aliwaagiza maafisa tarafa wa tarafa za Lukumbule na Nampungu kusimamia na kutatua mgogoro wa mipaka uliopo katika kijiji cha Machemba na Azimio.

Maagizo hayo yamekuja baada ya wananchi wa kijiji hicho kulalamika mbele ya mkuu wa wilaya juu yakuchukuliwa eneo lao na wananchi wa kijiji cha Machemba kwa muda mrefu huku ramani ya mipaka ikiwa ni tofauti na ile iliyotolewa na Idara ya Ardhi na Maliasili ya Halmashauri ya Tunduru.

Akitoa maelezo ya mgogoro huo wa mipaka katika kijiji hicho Ofisa Mtendaji wa kata ya Mtina Bi.Judith Mwamili alisema kuwa tatizo hilo limefanyiwa kazi na afisa ardhi na maliasili kwa kusoma ramani ya mipaka kwa kutumia GPS ili kutambua mipaka kuanzia mwaka 2016.

Alisema baada ya vipimo kufanyika eneo lenye mgogoro lilionekana kuwa ndani ya kijiji cha machemba lakini  uongozi wa kijiji cha Azimio walikataa ramani na kudai kuwa wanataka kutumia ramani ya mwaka 1979 badala ya ramani iliyoletwa na idara ya ardhi ya mwaka 2008.

Mkuu wa wilaya ya Tunduru Mhe.Juma Zuberi Homera akiongea na wananchi wa Kijiji cha Azimio ambao hawapo kwenye picha katika mkutano wa hadhara wa kuslikiliza na kutatua kero na changamoto za wananchi.

Naye mkuu wa wilaya ya Tunduru akaagiza vijiji vyote viwili yaani Machemba na Azimio kuunda kamati ya maridhiano itakayoshirikiana na maafisa tarafa na watumishi wa Idara ya Ardhi na Maliasili ndani ya mwezi mmoja ili kusuluisha mgogoro uliopo.

Aidha kwa upande wa kilimo katika skimu ya umwagiliaji ya madaba kwa baadhi ya mabanio kutokufanya kazi toka mradi kukabidhiwa kwa halmashauri mkuu wa wilaya Juma Homera alisema serikali inafanyia kazi kwa kushirikiana na wizara ya kilimo, ushirika na umwagiliaji kutatua changamoto iliyopo.

Mkuu huyo wa wilaya alisema kumekuwa na changamoto nyingi kwani mradi huo ulijengwa chini ya kiwango na sio huo tuu ila ni miradi yote katika skimu za Madaba, Kitanda, Misyaje na Lelolelo ilitekelezwa chini ya kiwango.

wananchi wa kijiji cha Azimio wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homera ambaye hayuko katika picha.

Serikali kwa kuliona hilo ili kuwasaidia wananchi marekebisho yatafanyika kupitia mradi wa ASDP II(Agricultural Sector Development Program) ili kuondoa changamoto kwa wananchi na kuokoa fedha zilizotumiwa na serikali katika kuendeleza kilimo cha umwagiliaji wilayani Tunduru na Tanzania kwa ujumla.

Mwisho.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.