• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

KURUGENZI SC yashiriki bonanza Nyerere day.

Imewekwa : October 15th, 2023

Halmashauri ya wilaya ya Tunduru ilishiriki Bonanza la michezo na Taasisi ya Mbesa Mission, ikiwa ni Maadhimisho ya kumbukumbu kifo cha Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Oktoba 14, katika viwanja vya Mbesa Mission.

Halmashauri ya wilaya ya Tunduru iliwakilishwa na timu ya Kurugenzi SC na taasisi ya Mbesa iliwakilishwa na CMML SC ,michezo mbalimbali ilichezwa ikiwemo Mpira wa Miguu, Mpira wa Wavu ,Mpira wa Pete , Mchezo wa bao na mchezo wa draft. 

Pichani ni wachezaji wa Kurugenzi SC (wenye jezi nyeupe)  wakishiriki Mpira wa Wavu.

Katika michezo yote hakupatikana mshindi wa Jumla kwani timu zote mbili zilifanikiwa kushinda michezo mitatu kati ya sita iliyochezwa, aidha katika mchezo wa Mpira wa Miguu Kurugenzi SC ilikubali kipigo cha Goli 1 dhidi ya CMML SC goli pekee lililofungwa na mshambuliaji wa CMML SC Nathanael Chilijila katika kipindi cha kwanza.

Aidha, katika michezo mingine ikiwemo Mpira wa pete Kurugenzi SC iliifunga CMML SC Goli 11 – 1, na mpira wa wavu Kurugenzi Fc kushinda kwa seti 2 kati ya seti 3 zilizopangwa kuchezwa, katika mchezo wa Bao Kurugenzi SC ilishinda michezo miwili kati ya mitatu iliyochezwa kwa upande wa draft kushindwa kwa michezo miwili dhidi ya CMML SC.

Akishukuru kwa niaba ya timu, Afisa Maendeleo ya Michezo Ndg, Abdilahi Namkopo amesema michezo ni sehemu ya kutengeneza mahusiano yenye tija miongoni mwa jamii, na kuhimiza kuwa uhusiano huu uliowekwa kuwa endelevu.

“Michezo ujenga umoja,ushirikiano na upendo baina yetu, kwahiyo kwa upande wetu tunashukuru kwa ukarimu mkubwa mliotuonyesha na kuhaidi kudumisha ushirikiano huu “. Alisema.

Kurugenzi SC inatarajia kuwaalika pia CMML SC katika mchezo wa marudiano utakaochezwa  viwanja vya nyumbani, ambapo tarehe ya Mchezo huo bado haijapangwa.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda, Kaimu Mkuu Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.