• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Kilimo cha Muhogo

Imewekwa : March 10th, 2018

Zao la muhogo ni zao la tatu kwa umaarufu na umuhimu wilayani Tunduru likitanguliwa na mazao ya korosho na mpunga. Mapema jana katika ukumbi wa skyway hapa wilayani Tunduru kulikua na warsha ya kilimo cha muhogo kwa kutumia mbegu za kisasa. Warsha hiyo iliandaliwa na Taasisi isiyo ya kiserikali ya  International Institute of Tropical Agriculture (IITA). Baadhi ya viongozi walioshiriki katika warsha hiyo ni wawezeshaji kutoka IITA, MEEDA, Wizara ya Kilimo Taasisi ya Utafiti Kibaha, Madiwani,  viongozi wa ngazi ya Halmashauri na wakulima wa mihogo wilayani Tunduru.

Akifungua warsha hiyo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ndg Jonathan A Haule alisema “Ili kukabiliana na baa la njaa, mabadiliko ya tabia ya nchi pamoja na hali ya wananchi wengi kutegemea mazao ya korosho na mpunga ni wakati sasa wa kubadilika na kuona umuhimu wa kuzalisha mazao mbalimbali ikiwemo uzalishaji wa muhogo kwa kutumia mbegu bora za kisasa” Aliendelea kwa kutaja faida za kilimo cha muhogo kuwa ni zao linalotumika  kwa chakula cha ugali, malighafi viwandani, kutengeneza maandazi, chapati, chipsi na ni zao linalostahimili ukame.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru ndugu Jonathan Haule (aliyesimama) akifungua warsha ya kilimo cha muhogo, kushoto kwake ni mwenyekiti wa Halmashauri ya wiliya  mh. Mbwana Mkwanda Sudi na anayefuta ni Makamu mwenyekiti wa Halmashauri mh. Mfaume Wadali.

Wawezeshaji hao kwa nyakati tofauti tofauti walieleza namna ya upatikanaji wa mbegu bora  za zao la muhogo, uandaaji wa mashamba, huduma, uvunaji na soko la zao hilo. 

Akizungumzia changamoto mwezeshaji kutoka IITA ndg Davis Mwakanyamale alibainisha baadhi ya magonjwa sugu yanayoshambulia zao hilo kuwa ni batobato na michirizi kahawia, na alitoa ushauri kwa wajumbe wa warsha hiyo kutumia mbegu bora  za mihogo kama Mkuranga 1, Kipusa, Chereko na Kizimbani ambazo zina uwezo mkubwa wa kuvumilia ukame pia kupambana na magonjwa na mabadiliko ya tabia ya nchi, uwezo wa kuzaa sana zaidi ya tani 20 kwa hekta pia ni mbegu zinazokomaa mapema.

Timu ya wawezeshaji wa warsha ya kilimo cha muhogo, kutoka kushoto ni Bi. Hellen Kiozya (wizara ya kilimo taasisi ya utafiti Kibaha) Bw.Davis mwakatumbula (IITA), 

Bw.Lokola Ndibalema  (IITA) na Bw. Erick Muhongole kutokea taasisi ya MEEDA

Nao madiwani walitoa mapendekezo ya baadhi ya mbinu za kuongeza uzalishaji wa zao hilo kuwa ni kutafuta soko la uhakika, kutoa elimu ya uzalishaji kwa wananchi kupitia maafisa ugani wa Kata na wananchi kuwezeshwa upatikanaji wa mbegu bora za kisasa kwa bei nafuu.

Aidha kwa umoja wao madiwani hao walikubaliana na umuhimu wa kuongeza uzalishaji wa zao hilo muhimu kwa chakula na biashara na kwamba kila mmoja ataenda kushawishi na kutoa Elimu kwa wananchi wake kuzalisha mbegu za mihogo bora kupitia vikundi vya wajasiliamali kwenye  kata zao ili kuwa na mashamba ya mfano.

Mwenyekiti wa Halmashauri  Wilaya ya Tunduru Mh. Mbwana Mkwanda Sudi alihitimisha warsha hiyo kwa kuwashukuru wawezeshaji, viongozi  na wadau kwa kusema “Halmashauri ina shauku ya kutimiza agizo la kuwa na viwanda vikubwa na vidogo vidogo vya  uzalishaji na usindikaji, na ili kutimiza adhma hii Halmashauri yetu itatilia mkazo  katika fursa hii kwa wakazi wa Wilayani Tunduru kuzalisha na  kuanzisha viwanda vya usindikaji wa muhogo kwa matumizi ya chakula na viwandani”.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru Mh. Mbwana Mkwanda Sudi akihitimisha warsha ya kilimo cha muhogo wilayani Tunduru.

Baadhi ya wajumbe waliohudhuria katika warsha ya kilimo cha muhogo wilayani Tunduru tarehe 09.03.2018


Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.