• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

Imewekwa : October 23rd, 2025



Serikali ya Wilaya ya Tunduru imeendelea kusisitiza umuhimu wa kudumisha amani na utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, sambamba na kuimarisha hatua za kudhibiti migogoro ya wakulima na wafugaji ambayo imekuwa ikijitokeza katika baadhi ya maeneo ya wilaya hiyo.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Kamati ya Usalama ya Wilaya, Viongozi wa Dini, Wazee Maarufu, Mamwenye, Masultani na Machifu, Maafisa Tarafa, Wakuu wa Idara, pamoja na viongozi wa makundi mbalimbali ya kijamii wakiwemo viongozi wa Bodaboda, Bajaj, Guta, AMCOS, Chama cha Mpira wa Miguu, Wasafirishaji na Wachimba Madini.


Akizungumza katika kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mheshimiwa Denis Masanja, ametoa wito kwa wananchi wote kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi ili kutekeleza haki yao ya kikatiba kwa amani, utulivu na kuzingatia sheria za nchi.


“Uchaguzi wetu utafanyika kwa amani na utulivu. Vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga kuhakikisha kila mwananchi anapata nafasi ya kupiga kura katika mazingira salama. Tunawaomba wananchi wajitokeze kwa wingi na kuepuka vitendo vyovyote vinavyoweza kuvuruga amani,” alisema Mhe. Masanja.


Aidha, kikao hicho kimejadili kwa kina changamoto ya migogoro kati ya wakulima na wafugaji, ambapo Mhe. Masanja alieleza kuwa serikali imeanza operesheni maalum ya kuwabaini na kuwaondoa wafugaji wanaoingiza mifugo kwenye maeneo yasiyoruhusiwa, kuvamia mashamba au kufanya uharibifu wa mazao ya wakulima.


 “Kila kijiji kina Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi unaoainisha maeneo ya kilimo, makazi na malisho. Wafugaji wanaoingia kinyume na mipango hiyo wanavunja sheria. Tumewakamata baadhi yao na hatua za kisheria zinaendelea. Hatutasita kumfikisha mahakamani yeyote atakayekiuka taratibu hizi,” alisisitiza DC Masanja.



Mhe. Masanja pia aliwaonya wananchi kuepuka kujichukulia sheria mkononi dhidi ya wafugaji wanaoingia kiholela katika maeneo yao, akisisitiza umuhimu wa kutoa taarifa kwa Kamati za Maridhiano za Vijiji au kwa viongozi wa Serikali za Mitaa mara wanapobaini uwepo wa mifugo isiyoruhusiwa.


 “Tunaendelea kufanya kazi bega kwa bega na vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha migogoro hii inakomeshwa. Tunawaomba wananchi wafuate sheria na kutoa taarifa mapema badala ya kujihusisha na vitendo vya kujichukulia hatua wenyewe,” aliongeza.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.