• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

KILELE cha maadhimisho ya siku ya usafishaji Duniani.

Imewekwa : September 16th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mheshimiwa Julius Mtatiro, akiwa ameambatana na Katibu Tawala wa Wilaya ya Tunduru Mh. Sanga Milongo,Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Tunduru ndg. Masanja Kengese, wakuu wa Taasisi mbali mbali, wakuu wa Idara pamoja na Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru wameazimisha Kilele cha Zoezi la Usafishaji wa mazingira Duniani.  

Katika zoezi hilo, Viongozi walishirikiana na wananchi katika kufanya usafi wa mazingira wakianzia Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru na maeneo mbali mbali ya Wilaya, ikiwa ni pamoja na barabara, mitaro, sokoni na maeneo ya biashara.

Akizungumza na wananchi waliotikia zoezi la usafishaji wa mazingira Mh. Mtatiro ameagiza idara ya mazingira kuhakikisha penye makutano ya mitaro kukaguliwa, kufanya kikao na wafanyabiashara wote ili kubaini changamoto zilizopo ndani ya siku 14.

“Usafi sio kazi ya Serikali na uchafu hauna kisingizio, mitaro ilindwe na ifanyiwe usafi, wekeni utaratibu wa kusimamiana ili yeyote anaemwaga uchafu ovyo kwenye mitaro ashughulikiwe, uchafu unadhibitika, niwaombe tusaidiane kuiweka Tunduru yetu katika hali ya usafi”. Alisema.

Akifafanua hilo Mh. DC Mtatiro alisema, Serikali imetimiza wajibu wake kujenga miundombinu ya Barabara na mifereji, hivyo amewaasa wananchi wawajibike kutunza mazingira yao.

Aidha ametoa agizo zoezi la usafi liwe endelevu, wafanyabiashara wote wawe na vifaa vya kuweka taka,vile vile, kila jumamosi ya mwisho wa mwezi iwe siku ya usafi, viongozi wa halmashauri watakuwa wakipita maeneo yote kwa ajili ya kuhimiza wananchi kufanya usafi.

Zoezi la usafishaji wa mazingira duniani kote lilianza mnamo Septemba 11, 2023, na kuhitimishwa mnamo Septemba 16, 2023, kauli mbiu ikiwa “Tuungane pamoja ,kujifunza,kupanga na kuhimiza uimalishaji huduma za udhibiti wa Taka"

Imeandaliwa na Orpa Kijanda,Kaimu Mkuu Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • VIWANJA vilivyopimwa vinauzwa. September 06, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2022/2023 July 24, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KWA WENYE VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA TUNDURU. September 07, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA TUNDURU. September 18, 2023
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • MAFUNZO ya Usimamizi endelevu wa Maliasili ya Jamii.

    September 22, 2023
  • JUKWAA la Wanawake lazinduliwa Tunduru.

    September 21, 2023
  • UBORESHAJI wa vyoo 2022/2023 Tunduru

    September 18, 2023
  • KILELE cha maadhimisho ya siku ya usafishaji Duniani.

    September 16, 2023
  • Ona Zote

Video

KUELEKEA Mnada wa Mwisho wa Mbaazi Tunduru.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.