• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

KIKAO cha uboreshaji Lishe Bora Tunduru.

Imewekwa : September 8th, 2023

Halmashauri ya wilaya ya Tunduru, imefanya kikao cha kujadili utekelezaji wa masuala ya Lishe kutoka idara mbalimbali na vitengo, kwa kipindi cha robo ya nne (April – Juni 2023), katika ukumbi wa Halmashauri  Agosti 8, 2023.

Kikao hiki kilikuwa na nia ya kuhakikisha kuwa mipango na Sera za Afya na Lishe zinatekelezwa kikamilifu ili kuboresha hali ya Lishe kwa Umma. Sera na mipango iliyofanikiwa mpaka sasa ni pamoja na kuongeza upatikanaji wa chakula bora na lishe bora kwa kila mtu, utoaji wa  Elimu juu ya afya na lishe bora, kuweka sera na sheria zinazosaidia kuboresha lishe, kuendeleza kilimo cha mazao bora kama vile viazi Lishe, kilimo cha Matunda na mboga mboga, kuongeza upatikanaji wa Maji safi na salama, kutoa matibabu ya utapiamlo.

Kamati ilijadili pia uanzishwaji wa bustani ya mboga mboga katika shule zote za Wilaya ya Tunduru, na ilibainika kuwa kati ya shule 29 za Sekondari, ni shule 5 tu ambazo bado hazijafikiwa na programu hiyo. Hatua zilipendekezwa kwa ajili ya kuhakikisha kuwa bustani hizo zinawekwa katika shule zote.

Pichani: Baadhi ya wajumbe wa Kikao Cha kamati ya Lishe.

 Afisa Lishe Wilaya ya Tunduru Bi. Martha Kibona alitolea ufafanuzi juu ya matumizi bora ya lishe ,hasa katika utumiaji wa chumvi yenye madini rutubishi kwa binadamu (Madini joto).

“Elimu inaendelea kutolewa kwa wananchi juu ya matumizi bora ya chumvi hususani kuwa makini na Chumvi ambayo haina madini  joto”.  Alisema.

Pichani: kutoka kushoto ni Afisa Lishe Wilaya ya Tunduru Bi. Martha Kibona akiwa na Mwandishi wa vikao Bi. Laiti Zuberi.

Kamati iliazimia kuhakikisha upatikanaji wa mbegu za viazi lishe kwa umma na kuwahimiza wadau kusambaza mbegu hizo sehemu zote za Halmashauri. Hatua hii inalenga kuboresha upatikanaji wa chakula chenye lishe bora kwa jamii yote.

Kwa kipindi cha robo ya nne, Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mjini Tunduru imezalisha maji na kusambaza kwa wateja Zaidi ya lita milioni 30 ambazo ni sawa na asilimia 50. Pia, imeendelea na kazi ya ukarabati na ujenzi wa miradi ya maji safi na salama Mjini Tunduru.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda,Kaimu Mkuu Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.