• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Jumuyia ya Tawala za mitaa Mkoa wa Ruvuma watakiwa kubuni vyanzo vipya vya mapato.

Imewekwa : May 20th, 2019


na Theresia Mallya-Tunduru

20/05/2019

Viongozi naombeni msimamie ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri zenu ili tuweze kufikia malengo tuliyojiwekea katika bajeti na kutekeleza mipango iliyop kwenye mpango wa bajeti wa mwaka 2018/2019 alisema Kaimu Katibu Tawala wilaya ya Tunduru Ndg.Augustine Maneno wakati akifungua mkutano wa Jumuiya Tawala za Mitaa ALAT Mkoa wa Ruvuma  uliofanyika wilayani Tunduru.

Ni wakati wa kubuni vyanzo vipya vya mapato na kuacha kutegemea katika mazao tuu kwani katika msimu mwaka 2018/2019 tumekutana na changamoto ya ukosefu wa masoko hivyo mkoa wetu kushindwa kufikia malengo.

Akitoa mfano wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru ambayo kwa kiasi kikubwa mapato ya ndani  inategemea katika mazao ya Korosho, Mbaazi na Mpunga Ndg Augustine Maneno alisema “korosho imenunuliwa na serikali hivyo Halmashauri za Tunduru na Namtumbo wamekosa mapato eneo hilo, ni wakati sasa kila Halmashauri kubuni vyanzo mbadala vya mapato badala ya kutegemea mazao ya kilimo pekee”

Mdau wa uzalishaji wa mbegu bora za Muhogo kutoka Shirika la MEDA akitoa maelekezo ya namna ya uandaaji wa shamba kwa wajumbe wa ALAT mkoa wa Ruvuma walipotembelea shamba la Mkulima mzalishaji wa mbegu Ndg Athmani Nkinde.

Kaimu Katibu Tawala huyo aliendelea kwa kuwataka wajumbe wa ALAT wa Ruvuma kusimamia na kufanya ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao ya utawala ili iwe na ubora na kuzingatia thamani ya fedha iliyotolewa, kwani serikali imetoa fedha nyingi sana zinazohitaji kutoa matokea chanya.

Aidha aliwataka wajumbe hao wanaporudi katika Halmashauri zao kuanzisha mpango mkakati wa benki tofali kwa kila kijiji ili kukabiliana na kutatua changamoto ya upungufu wa vyumba vya madarasa na kuboresha mazingira ya kujifunzia wanafunzi.

Alisema “tukiboresha miundombinu ya kujifunzia hata wanafunzi watapenda shule na kusoma kwa furaha, kama wakipenda shule basi hata kiwango cha ufaulu kitaongezeka katika shule za mkoa wa Ruvuma”

Kaimu mkurugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya ya Tunduru Bi Celestina Kahangwa ambaye pia ni Afisa Elimu Sekondari akitoa taarifa fupu ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa maktaba katika shule ya sekondari Masonya wakati wa ukaguzi wa miradi uliofanywa na wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa mkoa wa Ruvuma siku moja kabla ya kufanya Mkutano wa kujadili maendeleo ya mkoa wao.

Aliwakumbusha wajumbe kuwa sera ya serikali ya awamu ya Tano katika sekta ya Afya  ni kila kijiji kuwa na zahanati ili kurahisha utoaji wa huduma za afya kwa wananchi, nendeni mkawahamasishe wananchi kufyatua tofali na kuanza ujenzi wa zahanati kwa kila kijiji.

Kaimu Katibu Tawala alimalizia kwa kuwataka wajumbe wa ALAT mkoa wa Ruvuma kuwaalika wadua mbalimbali wanaotoa huduma katika mkoa wa Ruvuma katika vikao na mikutano ili kutoa elimu ya namna wanavyotoa huduma kwa wananchi kwa ajili ya maendeleo mapana ya mkoa wa Ruvuma.

Wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa walifanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika shule za sekondari Masonya ,ujenzi wa maktaba, Frankweston ukamilishaji wa maboma 2 na shamba la uzalishaji wa mbegu bora za mhogo aina ya Kiroba  lilipo kata ya sisi kwa sisi wilayani Tunduru.

Mwisho.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • SULUHU YA KUDUMU Maji Tunduru Yapatikana: Mkataba Wa Bilioni 3.2 Wasainiwa

    May 07, 2025
  • BODI Ya Wakurugenzi wa Mamlaka Ya Maji Na Usafi Wa Mazingira Tunduru (TUUWASA) Yazinduliwa

    May 07, 2025
  • TUNDURU Yajizatiti Kukabiliana na Ugonjwa wa Mpox.

    March 27, 2025
  • TUNDURU Yaungana katika Dua na Iftar

    March 24, 2025
  • Ona Zote

Video

WANANCHI WAENDELEA KUPATIWA MAFUNZO KWA VITENDO ILI KUTATUA MIGONGANO YA BINADAMU NA WANYAPORI.
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.